Sports
Uganda Cranes Kileleni Kundi C Michuano Ya CHAN
Timu ya taifa ya Uganda, maarufu kama Uganda Cranes, imekwea kileleni mwa Kundi C baada ya ushindi wa mabao 2–1 dhidi ya Niger jana kwenye uwanja wa Nelson Mandela, mjini Kampala.
Mshambulizi nyota na nahodha Allan Okello aliwaweka Uganda Cranes kifua mbele dakika ya 21, dakika chache baada ya kupoteza nafasi ya penalti, kabla ya mshambulizi Joel Sserunjji kuongeza bao la pili dakika ya 56 kipindi cha pili.
Huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa wenyeji wenza wa CHAN, baada ya kuanza kwa kusuasua walipopoteza mechi ya ufunguzi kwa mabao 3–0 dhidi ya Algeria, maarufu kama The Desert Foxes.
Uganda sasa ina alama 6 baada ya michezo mitatu, ikifuatiwa na Algeria yenye alama 4, Afrika Kusini ikiwa nafasi ya tatu pia na alama 4, Guinea ikishika nafasi ya nne na alama 3, huku Niger ikiburuza mkia bila pointi yoyote kwenye michezo ya kundi hilo.
Entertainment
Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy
Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.
Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.
Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.
“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.
Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.
Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.
Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.
Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

