Connect with us

News

Wataalam wa Uchumi wa Bahari washinikiza Viongozi kuwawezesha Wananchi.

Published

on

Wataalamu wa sekta ya uchumi wa samawati na maswala ya bahari hapa nchini wamesistiza haja ya serikali kuweka mazingira bora ya kubuni nafasi zaidi ya ajira ili kuinua uchumi wa bahari.

Mtaalam wa sekta hiyo Stanley Chai alisema uboreshaji wa mazingira ya sekta hiyo utachangia waekezaji zaidi kuekeza hapa nchini.

Chai alidokeza kuwa bahari hindi inafursa kubwa ya kuinua uchumi wa nchi kutokana na raslimali zinazopatikana bahari hindi.

“Nilazima tuweke mazingira yakuvutia meli nyingi, hii bahari yetu kuna mda ukiangalia kuna meli hamsini zinapita, tumekuwa tukishauri ulimwengu na kinachofanyika ni kuweka mazingira ya kuekeza upatikanaji wa samaki wa kiviwanda nchini, kama saa hii Kenya mtu akitaka liseni ya kwenda kuvua samaki kama hivi tuna tunamtoza dola elfu hamusini kwa mwaka”,alisema Chai.

Kuhusu swala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa za samaki kutoka taifa la uchina katika soko la hapa nchini, mtaalam huyo alisema uhaba wa samaki hapa nchini umechangia uendelezaji wa biashara baina ya nchi hizo mbili ili kutosheleza lishe miongoni mwa jamii nchini.

 “Japan ndio walaji wakubwa wa samaki ulimwenguni, samaki wakiletwa hapa ndio wavuvi wetu watafaidi, wakati samaki wanapelekwa nje ujue samaki wetu wenye thamani ndio wanaenda nje na sisi tunakula tilapia ambao wameletwa kutoka huko, kama samaki wangekuwa wanatutosheleza hapa hakungekuwa na soko la wachina, lakini kwa sababu hawatutoshelezi ndio maana watu wamepata mwanya wa kuleta”, aliongeza mtaalam huyo.

Mtaalam wa maswala ya uchumi wa bahari Stanley Chai akipokezwa zawadi na Coco fm.

Wakati huo huo alishinikiza viongozi hapa nchini kutafuta ufahamu zaidi kuhusu maswala ya uchumi wa bahari sawa na kuweka mikakati ya kubuni nafasi za ajira ili kuwezesha wananchi kimaendeleo.

“Haieleweki kama wewe ni mbunge unasema utaendeleza eneo bunge lako na CDF ya shilingi milioni 170, hakuna maendeleo utaleta, kwa hivyo vingozi tunafaa kufikiria tofauti, tuje na njia mbadala ya kwamba tutabuni ajira na tutaleta utajiri watu wajitegemee na njia moja rahisi ni hii, sisi tunashukuru sana rais alisikiza akaelewa na kwa mara ya kwanza akaunda wizara nzima ya uchumi samawati, ninini tena unataka? Unataka kumlaumu rais tena?”, aliuliza Chai.

Tamko la mtaalam huyo linajiri wakati Kenya ikiadhimisha sherehe za miaka 62 za siku ya madaraka, ambazo ziliongozwa na rais William Ruto katika kaunti ya Homabay huku kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ikiwa ni “Uchumi sanawati na maswala ya bahari”.

Taarifa na Joseph Jira

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Sakata ya mafuta yaathiri sekta ya uchukuzi nchini

Published

on

By

Huenda watumizi wa magari ya uchukuzi wa umma, wahudumu wa tuktuk na bodaboda wakalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na changamoto za ukosefu wa mafuta nchini na kuathiri zaidi shughuli za uchukuzi.

Hatua hii imetakana na changamoto za uhaba wa mafuta nchini baada ya kuibuka kwa sataka ya uagizaji wa mafuta ghushi kupitia bandari ya Mombasa.

Kulingana na serikali kupitia Wizara ya Kawi, sakata hiyo ya shilingi bilioni 12 ilikuwa imelata tani elfu 60 za mafuta ya petroli kinyume cha sheria pamoja na mipango ya serikali ya uagizaji mafuta wa serikali kwa serikali yaani G to G.

Sakata hii imepelekea Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti kawi na bei za mafuta nchini EPRA Daniel Kiptoo, Katibu katika Idara ya petroli nchini Mohammed Liban na mkurugenzi wa Kampuni ya Kenya Pipeline Joe Sang kujiuzulu.

Kujiuluzu kwao kumetokana na kukamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, kwa ushirikiano na Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC baada ya kutilia shaka zabuni iliyopewa kampuni binafsi ya One Petroleum Limited inayomilikwa na mfanyibiashara mashuhuri jijini Mombasa.

Wahudumu wa sekta ya bodaboda wakikabiliwa na changamoto za uhaba wa mafuta ya Petroli

Siku ya Jumanne, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandanyi alifanya kikao na wakurugenzi wa kampuni za mafuta nchini na kuagiza shehena ya mafuta katika bandari ya Mombasa kurejeshwa kwani serikali haitambua shehena hiyo.

“Wahusika wa sakata hiyo walikuwa na njama ya kuongeza bei ya mafuta nchini kwa shilingi 14 zaidi kwa lita wakitumia nafasi ya vita vinavyoendelea kati ya Iran na Marekani na Israel, hiyo hatuta kubali”, alisema Wandayi.

Hatua hiyo ilikuwa inalenga pia kukwepa mpango wa serikali wa uagizaji mafuta kutoka mataifa ya miliki za kiarabu wa serikali kwa serikali yaani G to Go, akisema wahusika wa sakata ya ufisadi ni lazima wachukuliwe hatua.

Itakumbukwa kwamba rais William Ruto hivi majuzi alidokeza kwamba wahusika wote wa sakata ya ufisadi kwenye sekta ya mafuta watachukuliwa hatua, akishililia kwamba serikali haitakubali ufisadi nchini, huku akikosa kuweka wazi hatma ya maafisa hao wakuu wa serikali.

“Hawa walaghai wa mambo ya mafuta watakipata, hawaweze kuhepa kwa sababu haiwezekani katika taifa letu la Kenya watu wanaone tuko na shida ya mashariki ya kati wanakuja kukoroga shida nyengine hapa Kenya, serikali itakabiliana kikamilifu na wafisadi”, alisema Rais Ruto.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Buriani Mama Dorothy Baya, 1947-2026

Published

on

By

Mwili wa Mama Dorothy Baya Mweri ambaye ni Mama mzazi wa bunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya umetolewa katika makafani ya hospitali ya rufaa ya Kilifi kaunti ya Kilifi.

Mwili wa Mama Dorothy umefanyiwa ibada fupi ya wafu nje ya makafani ya hospitali hiyo ikiongozwa na viongozi wa kidini kisha wananchi wakapata fursa ya kuutazama mwili ili kutoa heshima yao ya mwisho kwa marehemu.

Viongozi mbalimbali wa kisiasa pia walikuwa na nafasi ya kumpa mkono wa buriani Mama Dorothy wakiongozwa na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro na Mwenyekiti wa bodi ya hazina ya michezo na sanaa ambaye pia ni mgombea wa wadhfa wa useneta kaunti ya Kilifi Wakili George Kithi.

Viongozi wengine waliokuwepo kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu ni pamoja Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mgombea wa wadhfa wa uwakilishi wa kike kaunti ya Kilifi Christine Zawadi, miongoni mwa wengine.

Msafara wa Marehemu baadaye ulielekea katika kijiji cha Dabaso eneo bunge la Kilifi Kazkani kaunti ya Kilifi kwa ibada ya misa ya wafu katika Kanisa la St Stephen Dabaso kabla ya halfa ya mazishi siku ya Jumatatu.

Msafara wa Marehemu Mama Dorothy Baya ukielekea katika kijiji cha Dabaso eneo bunge la Kilifi Kazkani kaunti ya Kilifi kwa hafla ya mazishi.

Marehemu amewaacha watoto 6, akiwemo Mbunge wa Kilifi Kazikazini ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa wengine bungeni Owen Baya, Askofu mkuu wa Kanisa la Kianglikana Dayosi ya Mombasa Alphonce Mwaro,Charity Mapenzi, Felix Mweri, Mercy Kadii na Catherine Harusi, pamoja na wajuu kadhaa.

Hata hivyo viongozi na wananchi wa tabaka mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria halfa ya mazishi ya Mama Dorothy itakayofanyika siku ya Jumatatu hapo kesho tarehe 6 mwezi Aprili mwaka huu katika kijiji cha Dabaso.

Mama Dorothy aliaga dunia tarehe 30 mwezi Machi, 2026.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending