News
Wataalam wa Uchumi wa Bahari washinikiza Viongozi kuwawezesha Wananchi.
Wataalamu wa sekta ya uchumi wa samawati na maswala ya bahari hapa nchini wamesistiza haja ya serikali kuweka mazingira bora ya kubuni nafasi zaidi ya ajira ili kuinua uchumi wa bahari.
Mtaalam wa sekta hiyo Stanley Chai alisema uboreshaji wa mazingira ya sekta hiyo utachangia waekezaji zaidi kuekeza hapa nchini.
Chai alidokeza kuwa bahari hindi inafursa kubwa ya kuinua uchumi wa nchi kutokana na raslimali zinazopatikana bahari hindi.
“Nilazima tuweke mazingira yakuvutia meli nyingi, hii bahari yetu kuna mda ukiangalia kuna meli hamsini zinapita, tumekuwa tukishauri ulimwengu na kinachofanyika ni kuweka mazingira ya kuekeza upatikanaji wa samaki wa kiviwanda nchini, kama saa hii Kenya mtu akitaka liseni ya kwenda kuvua samaki kama hivi tuna tunamtoza dola elfu hamusini kwa mwaka”,alisema Chai.
Kuhusu swala la kudhibiti uingizaji wa bidhaa za samaki kutoka taifa la uchina katika soko la hapa nchini, mtaalam huyo alisema uhaba wa samaki hapa nchini umechangia uendelezaji wa biashara baina ya nchi hizo mbili ili kutosheleza lishe miongoni mwa jamii nchini.
“Japan ndio walaji wakubwa wa samaki ulimwenguni, samaki wakiletwa hapa ndio wavuvi wetu watafaidi, wakati samaki wanapelekwa nje ujue samaki wetu wenye thamani ndio wanaenda nje na sisi tunakula tilapia ambao wameletwa kutoka huko, kama samaki wangekuwa wanatutosheleza hapa hakungekuwa na soko la wachina, lakini kwa sababu hawatutoshelezi ndio maana watu wamepata mwanya wa kuleta”, aliongeza mtaalam huyo.

Mtaalam wa maswala ya uchumi wa bahari Stanley Chai akipokezwa zawadi na Coco fm.
Wakati huo huo alishinikiza viongozi hapa nchini kutafuta ufahamu zaidi kuhusu maswala ya uchumi wa bahari sawa na kuweka mikakati ya kubuni nafasi za ajira ili kuwezesha wananchi kimaendeleo.
“Haieleweki kama wewe ni mbunge unasema utaendeleza eneo bunge lako na CDF ya shilingi milioni 170, hakuna maendeleo utaleta, kwa hivyo vingozi tunafaa kufikiria tofauti, tuje na njia mbadala ya kwamba tutabuni ajira na tutaleta utajiri watu wajitegemee na njia moja rahisi ni hii, sisi tunashukuru sana rais alisikiza akaelewa na kwa mara ya kwanza akaunda wizara nzima ya uchumi samawati, ninini tena unataka? Unataka kumlaumu rais tena?”, aliuliza Chai.
Tamko la mtaalam huyo linajiri wakati Kenya ikiadhimisha sherehe za miaka 62 za siku ya madaraka, ambazo ziliongozwa na rais William Ruto katika kaunti ya Homabay huku kauli mbiu ya maadhimisho ya sherehe za mwaka huu ikiwa ni “Uchumi sanawati na maswala ya bahari”.
Taarifa na Joseph Jira
News
Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni
Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali
Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.
Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.
Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.
Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.
Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke
Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.
Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.
Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.
Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.
Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.
Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.
Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

