Connect with us

News

Watene: CBC itawafaidi wakenya iwapo itaangazia changamoto za wananchi.

Published

on

Mgombea wadhifa wa urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2027 Robert Watene amesema mfumo wa mtaala wa elimu nchini CBC utawafaidi wakenya iwapo utaangazia changamoto wanazokumbana nazo wakenya.

Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na Coco FM, Watene amesema nchi ya Kenya imesalia nyuma kielimu na kimaendeleo tofauti na nchi zingine kwani mfumo uliyopo nchini haujampa mtoto ujuzi wa kumasaidia kujiajiri baada ya masomo.

Akitolea mfano nchi ya Ujerumani, Watene amesema mfumo wao huangazia kuwapa wanafunzi ujuzi jambo ambalo kulingana naye limepunguza ongezeko la ukosefu wa ajira nchini humo.

“Masomo ya nje wanafocus sana na problem za kwao hata ukiangalia zile curriculum zao zinajaribu kusolve zile matatizo ambazo wako nazo unapata mtu amemaliza kusoma na tayari ako na skill ya kutengeneza magari na kadhalika” alisema Robert Watene.

Watene amesema mfumo mpya wa CBC unastahili kuwa kama vyuo vya kiufundi ili kuwasaidia vijana kujiajiri pindi tu wanapokamilisha masomo yao.

Wakati uo huo amesema iwapo atapata nafasi ya kuongoza taifa la Kenya atahakikisha anabadilisha maji ya bahari kuwa maji safi kwa matumizi ya binadamu ili kuwapunguzia dhiki wakaazi wa eneo la Pwani.

“There people who are walking kilometers and kilometers to get water ila hakuna kiongozi ambaye amesimama kuhakikisha kwamba haya maji yetu ya bahari yanageuka maji safi ya kunywa ili kupunguza magonjwa yanayosababishwa na maji chafu” alidokeza Watene.

Taarifa ya Elizabeth Mwende.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending