Connect with us

Sports

Mornings Stars na Kilifi Elite Ndiyo Mabingwa Makala ya Tatu Kombe la Esse Akida

Published

on

Toleo la tatu la Mashindano ya Esse Akida lilifikia tamati Jumapili tarehe 28 Desemba 2025, huku Morning Stars na Kilifi Elite wakitawazwa mabingwa.

Mashindano hayo yaliyoandaliwa na mshambuliaji wa Harambee Starlets, Esse Akida, yalishirikisha jumla ya timu 19 katika kipengele cha wavulana na timu sita za wasichana, zilizocheza kwa mfumo wa ligi (round robin). Fainali za mashindano hayo zilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Masuala ya Vijana na Uchumi wa Ubunifu, Fikirini Jacobs, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Pia walikuwepo kocha mkuu wa Kibera Women Soccer FC, Bob Okallo, pamoja na nahodha wa Harambee Starlets na mwenzake Akida, Mwanahalima Jereko Adam, miongoni mwa wageni mashuhuri.

Akizungumza baada ya kukamilika kwa mashindano hayo, Akida alisema:
“Lengo langu tangu kuanzishwa kwa mashindano haya limekuwa kuwapa jukwaa wasichana na wavulana hawa chipukizi kuonyesha vipaji vyao.

“Tumeona maendeleo tangu tulipoanza, kwani baadhi ya washiriki wetu wa awali sasa wako kwenye timu mbalimbali, lakini tungependa kuona wengi zaidi wakijiunga na timu kubwa ili waweze kujipatia kipato kupitia vipaji vyao.”

Akida pia alisisitiza umuhimu wa washirika na marafiki waliotoa mchango mkubwa kufanikisha mashindano hayo.

“Ningependa kutoa shukrani za dhati kwa mshirika wetu mkuu MozzartBet kwa msaada wao mkubwa. Wamekuwa wakisaidia jamii mbalimbali na ninaamini wana mipango mikubwa zaidi kwa soka. Pia nina marafiki waliotoa mchango wao kwa kiwango kikubwa, na nawapongeza binafsi kwa kuhakikisha mashindano haya yamefanikiwa,” aliongeza Akida.

Muhtasari wa Mashindano

Makundi ya Wavulana

Kundi A
Makion
Mavueni
Young Atomic
Berets
United Spark

Kundi B
Mtondia
Kilifi Allstars
FC Talanta
Blue Blue
Matsangoni

Kundi C
Bofa
Ngala
Jupiter
Bahari
Kibaoni United

Kundi D
St Patrick’s
Ubuntu
Wavuvi
Morning Stars

Wanawake (Mfumo wa Ligi)
Majajani Queens
Bahari Starlets
Kilifi Elite
Kilifi Ladies
Bofa Starlets

Tuzo za Wachezaji Binafsi – Wanawake

Mfungaji Bora: Laureen Shoka (Bahari Starlets)
Mchezaji Bora: Rita Mwanaisha maarufu kama Toto (Kilifi Elite)
Kipa Bora: Nelly Chivatsi (Bahari Starlets)
Tuzo ya Mshikamano wa Timu (Team Spirit): Juliet Mapenzi (Kilifi Ladies)
Mchezaji Mdogo Zaidi: Asma Taura (Majajani Queens)
Mchezaji Aliyeonyesha Juhudi Bora: Asia Ali (Kilifi Elite)


Tuzo za Wachezaji Binafsi – Wanaume

Mfungaji Bora: Radigo Phiabian (Ubuntu)
Mchezaji Bora: Samuel Samini (Ubuntu)
Kipa Bora: Dida Ahmed (Morning Stars)


Tuzo za Timu – Wanawake

Nafasi ya 5: Bofa Starlets
Nafasi ya 4: Majajani Queens
Washindi wa Nafasi ya Tatu (2nd Runners Up): Kilifi Ladies
Washindi wa Nafasi ya Pili (1st Runners Up): Bahari Starlets
Mabingwa: Kilifi Elite


Tuzo za Timu – Wanaume

Nafasi ya 4: Mtondia United
Washindi wa Nafasi ya Tatu (2nd Runners Up): Blue Blue
Washindi wa Nafasi ya Pili (1st Runners Up): Ubuntu
Mabingwa: Morning Stars

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy

Published

on

Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.

Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.

Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.

“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.

Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.

Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.

Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.

Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

Continue Reading

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Trending