Connect with us

Editor's Picks

Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.

Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.

Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.

Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.

Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.

Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.

Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Editor's Picks

Uamuzi wa Kesi dhidi ya kampuni ya Mayport Limited Wahairishwa

Published

on

Photo: Courtesy

Mahakama ya ardhi na mazingira katika kaunti ya Mombasa imeahirisha uamuzi wa kesi dhidi ya kampuni ya Mayport Limited inayohusishwa na mfanyabishara maarufu Mohamed Jaffar.

Mlalamishi katika kesi hiyo Juma Abdhallah Munyao amesema kampuni hiyo ilinyakua ardhi yake yenye thamani ya mamilioni ya pesa kinyume cha sheria.

Jaji Titus Naikuni, amesema amechukua hatua hiyo baada ya Wakili wa mlalamishi Steve Ogola kupitia kwa njia ya mtandao kueleza Mahakama kwamba alichelewa kuwasilisha majibu ya upande wa mlalamishi, akisema alikuwa mgonjwa.

Wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo mwaka jana, Jaji Naikuni aliagiza kampuni ya Mayport Limited kupitia Wakili Shaniz Chatur na msaidizi wa Jaffar, Yakatali Amirali kuwasilisha hati miliki walizonazo kuthibitisha umiliki wa kipande hicho cha ardhi kinachozozaniwa.

Hata hivyo, wawili hao walishindwa mara kadhaa kuwasilisha stakabadhi hiyo mbele ya Mahakama pamoja na nyaraka zozote za malipo ya ununuzi wa ardhi hiyo huku walalamishi Juma Abdallah Munyao na Asma Nduku wakiwasilisha hati miliki halisi mbele ya Mahakama.

Hata hivyo Jaji Naikuni amesema pande zote mbili zitajulishwa tarehe ya uamuzi wa kesi hiyo.

Continue Reading

Trending