Connect with us

News

Ethekon: Uchaguzi mkuu utakuwa huru na haki, 2027

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imewahakikishia wakenya kwamba uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027 kutakuwa huru na wa haki kwani tume hiyo imejipanga kikamilifu.

Mwenyekiti wa Tume hiyo Erastus Ethekon aliyataka mashirika mbalimbali ya kijamii kushirikiana ili kuhakikisha uchaguzi huyo unakuwa huru na haki.

Akizunguza katika kongamano lililowaleta pamoja washikadau mbalimbali mjini Mombasa, Ethekon aliwahimiza vijana na waundaji maudhui mitandaoni kupeperusha habari za ukweli ili kuepuka taharuki miongoni mwa jamii.

“Nawahimiza baadhi yenu muwe makini hawa ambao ni Wananbloga kulingana na athari wako naye wakati wa uchaguzi na tusikubali kutumiwa vibaya kwa ajali ya michakato ya kidemokrasia,” alisema Ethekon.

Kwa upande wake Naibu Mwenyekiti wa Tume ya IEBC Fahima Abdallah alihimiza amani kwa jamii, akisema kupiga kura ni haki ya kila mkenya na ni muhimu kutekeleza suala hilo bila vurugu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wanaomiliki silaha haramu kaunti ya Tana river waonywa

Published

on

By

Idara ya usalama kanda ya Pwani imewaonya wananchi wanaomiliki silaha haramu katika kaunti ya Tana river.

Mshirikishi wa utawala kanda ya Pwani Paul Rotich aliwataka wanaomiliki silaha hizo kuzisalimisha mara moja kwa maafisa wa polisi katika kituoc cha polisi kiilichokaribu nao.

Akizungumza katika kikao cha kiusalama kaunti ya Tana river, Rotich alisema oparesheni ya kusaka silaha hizo imeenzishwa huku akiwaagiza machifu na manaibu wao kushirikiana na maafisa wa polisi ili kuhakikisha silaha hizo zinapatikana.

Rotich alisema zaidi ya bunduki 120 ziko mikononi mwa raia wa maeneo ya Bangale na Tana Kaskazini katika kaunti ya Tana river, akisema ni lazima zirudishwe kwa serikali.

“Tunataka zile bunduki zote mnazomiliki kinyume cha sheria mrudishe kwanza ndio tuongee mambo ingine, haiwezekana mnamiliki bunduki haramu na mnataka serikali iwalinde kwani mtaishi na majangili mpaka lini, hiyo maneno hatutakubali rudisheni bunduki ama tutaanzisha oparesheni kali”, alisema Rotich.

Hata hivyo wakaazi wa kaunti hiyo wamepongeza hatua hiyo ya serikali, wakiwarai wenyeji kukumbatia amani ili kuepuka umwagikaji wa damu katika kaunti hiyo.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mahakama kuu yamzuia Kingi na Wetangula kujihusisha na siasa

Published

on

By

Spika wa bunge la Kitaifa Moses Wetangula na spika wa bunge la Seneti Amason Kingi wamepigwa breki kujihusisha na mikutano ya kisiasa.

Hii ni kufuatia amri ya Mahakama kuu inayowataka wawili hao kukoma kujihusisha na uhamasishaji wa kisiasa kwa muda wakisubiri kusikilizwa kwa ombi linalopiga shughuli zao lilowasilishwa Mahakamani na Shirika la Vocal Africa.

Jaji wa Mahakama hiyo David Mburu, alitoa amri hiyo akiagiza kuwa ombi hilo lisikilizwe kwa umakini na washtakiwa wote wawasilishiwe stakabadhi za kesi hii leo.

Katika ombi hilo, Shirika la Vocal Africa linadai kuwa ushiriki wa maspika hao katika shughuli za kisiasa unaibua maswali mazito ya kikatiba kuhusiana na uhuru wa bunge na majukumu yaliyowekwa kwa maafisa wa serikali.

Vocal Africa pia limesisitiza kuwa, ingawa kila ana haki ya kuwa na maoni ya kisiasa na kushiriki katika maswala ya kisiasa, maspika wanashikilia ofisi za kikatiba ambazo hazihitaji upendelea bali zinahitaji uhuru wa kitaasisi.

Kwa muda sasa spika Kingi na Wetangula wameonekana katika mikutano mbalimbali ya kisiasa wakipigia debe ajenda ya rais William Ruto, kinyume na Katiba inayowalazimisha maspika kuangazia masuala ya bunge na shughuli zengine muhimu za kiserikali.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending