Connect with us

News

Furaha Chengo:Sijaagizwa nijiondoe kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo Magarini

Published

on

Mgombea wadhifa wa ubunge katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kupitia chama cha DCP Furaha Chengo Ngumbao almaarufu Kalama Wehu, amekana kupokea maagizo ya kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo eneo hilo la Magarini ulioratibiwa kufanyika mwezi Novemba 27, 2025.

Katika mahojiano kwenye kipindi cha Coco asubuhi, Kalama Wehu aliseme hajapokea maagizo yeyote ana iwapo hilo litatokea, ataendelea na harakati zake za kugombea wadhifa huo.

Matamshi ya Chengo yanajiri kufuatia madai kuwa mgombea huyo aliagizwa ajiondoe kwenye kinyang’anyiro hicho kutokana na kesi inayomkabili mahakamani.

Mwanaharakati huyo wa kisiasa alisema anaimani ya kuibuka na ushindi katika uchaguzi huo mdogo japo wapinzani wake wamekuwa wakitumia mbinu fiche za kuhujumu harakati zake za kuwania kiti hicho.

“Sijawahi kuitwa na mambo kama hayo na nikiitwa sinitakuwa nimeitwa? na uamuzi utakuwepo? wa kwamba mimi sishuki na nikishuka nitashuka na watu wa Magarini, yaani wanatafuta mbinu yeyote na walinitega kutoka kitambo, hii kushikwa na kufungwa vitu ambavyo havina hata kesi vimekuwepo kwa sababu wakiangalia watu mashinani wamewakataa”,alisema Chengo.

Wakati huo huo Chengo aliahidi kuboresha uchumi wa eneo hilo iwapo ataibuka na ushindi, kwa kuondoa ada za mashamba ili kuwapa nafasi wakaazi kujiendeleza kiuchumi kupitia kilimo.

“Kutoka mimi nizaliwe Magarini uchumi ulioko pale ni ule wa chumvi pekeyake ilihali tuko na nafasi ya kuwekeza viwanda vingi sana pale ndani ya Magarini, kuna sehemu zimefika umeme, zimefika barabara, zimefika maji, kumaanisha kwamba tukiweka viwanda vinaweza kufanya vizuri na wakaazi wapate ajira”,aliongeza mwanaharakati huyo.

Furaha Chengo alikamatwa kwa madai ya kuhusika katika maandamano ya kizazi cha Gen Z ya tarehe 25 mwezi Juni 2025, yaliyofanyika mjini Malindi na kusababisha vurugu zilizopelekea kuvunjwa kwa jengo la Al Noor, kunakopatikana makao makuu ya Ofisi za NSSF tawi la Malindi.

Uchaguzi huo mdogo unatarajiwa kuwa na ushindani makali baada ya vyama vya kisiasa kuwakabidhi vyeti wagombea wao waliotangaza nia ya kuwania wadhfa wa ubunge wa Magarini.

Katika uchaguzi huo mdogo, bendera ya chama cha ODM itapeperusha Harrison Garama Kombe anayelenga kutetea kiti chake baada ya ushindi wake kubatilishwa na Mahakama kuu.

Harrison Kombe anayegombea wadhfa wa ubunge Magarini kupitia chama cha ODM.

Chama cha Wiper kilimpa cheti Samuel Nzai kuwania wadhfa huo, huku chama cha UDA kikiwakilishwa na Stanley Karisa Kenga.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wajumbe wa bunge la Seneti wazuru kaunti ya Kilifi

Published

on

By

Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi na kupokelewa na Karani wa bunge hilo Michael Ngala.

Wajumbe hao wa sekta mbalimbali wa bunge la Seneti wakiongozwa na Daniel Chania, wametathmini masuala mbalimbali ya bunge la kaunti ya Kilifi kama lina uwezo wa kuandaa ziara ijayo ya Seneti mashinani.

Seneti Mashinani ilianzishwa chini ya kifungu cha 126 ibara ya kwanza ya Katiba ya Kenya ya mwaka 2010, kinachoruhusu kikao cha bunge lolote kufanyika mahali popote ndani ya taifa la Kenya na kuanza wakati wowote kitakapopangwa na bunge.

Malengo ya vikao hivyo katika kaunti ni pamoja na kuhamasisha umma kuhusu kazi za bunge na Seneti, kuimarisha ushiriki wa umma katika shughuli za Seneti kwenye ngazi ya kaunti sawa na kutoa hamasa kwa wananchi kwa lengo la kuhimiza ushiriki umma katika utawala.

Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi

Bunge la Seneti limeanza maandalizi ya vikao vitakavyofanyika nje ya Nairobi, ambavyo vinatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2026.

Kaunti ya Kilifi ni miongoni mwa kaunti zilizoteuliwa kuwa kati ya zile zitazoandaa vikao hivyo kwa ajali ya umma kuwa na uelewa zaidi kuhusu shughuli za bunge hilo.

Wajumbe hao walikuwa na malengo pia ya kubaini upatikanaji wa miundombinu na huduma muhimu ili kuiwezesha Seneti kufanya uamuzi.

Kaunti nyingine zilizowahi kuandaa Seneti Mashinani ni pamoja na kaunti ya Uasin Gishu mwaka 2018, ikifuatiwa na kaunti ya Kitui mwaka 2019, kaunti ya Turkana mwaka 2023 na kaunti ya Busia mwaka 2025.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Sakata ya mafuta yaathiri sekta ya uchukuzi nchini

Published

on

By

Huenda watumizi wa magari ya uchukuzi wa umma, wahudumu wa tuktuk na bodaboda wakalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na changamoto za ukosefu wa mafuta nchini na kuathiri zaidi shughuli za uchukuzi.

Hatua hii imetakana na changamoto za uhaba wa mafuta nchini baada ya kuibuka kwa sataka ya uagizaji wa mafuta ghushi kupitia bandari ya Mombasa.

Kulingana na serikali kupitia Wizara ya Kawi, sakata hiyo ya shilingi bilioni 12 ilikuwa imelata tani elfu 60 za mafuta ya petroli kinyume cha sheria pamoja na mipango ya serikali ya uagizaji mafuta wa serikali kwa serikali yaani G to G.

Sakata hii imepelekea Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti kawi na bei za mafuta nchini EPRA Daniel Kiptoo, Katibu katika Idara ya petroli nchini Mohammed Liban na mkurugenzi wa Kampuni ya Kenya Pipeline Joe Sang kujiuzulu.

Kujiuluzu kwao kumetokana na kukamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, kwa ushirikiano na Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC baada ya kutilia shaka zabuni iliyopewa kampuni binafsi ya One Petroleum Limited inayomilikwa na mfanyibiashara mashuhuri jijini Mombasa.

Wahudumu wa sekta ya bodaboda wakikabiliwa na changamoto za uhaba wa mafuta ya Petroli

Siku ya Jumanne, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandanyi alifanya kikao na wakurugenzi wa kampuni za mafuta nchini na kuagiza shehena ya mafuta katika bandari ya Mombasa kurejeshwa kwani serikali haitambua shehena hiyo.

“Wahusika wa sakata hiyo walikuwa na njama ya kuongeza bei ya mafuta nchini kwa shilingi 14 zaidi kwa lita wakitumia nafasi ya vita vinavyoendelea kati ya Iran na Marekani na Israel, hiyo hatuta kubali”, alisema Wandayi.

Hatua hiyo ilikuwa inalenga pia kukwepa mpango wa serikali wa uagizaji mafuta kutoka mataifa ya miliki za kiarabu wa serikali kwa serikali yaani G to Go, akisema wahusika wa sakata ya ufisadi ni lazima wachukuliwe hatua.

Itakumbukwa kwamba rais William Ruto hivi majuzi alidokeza kwamba wahusika wote wa sakata ya ufisadi kwenye sekta ya mafuta watachukuliwa hatua, akishililia kwamba serikali haitakubali ufisadi nchini, huku akikosa kuweka wazi hatma ya maafisa hao wakuu wa serikali.

“Hawa walaghai wa mambo ya mafuta watakipata, hawaweze kuhepa kwa sababu haiwezekani katika taifa letu la Kenya watu wanaone tuko na shida ya mashariki ya kati wanakuja kukoroga shida nyengine hapa Kenya, serikali itakabiliana kikamilifu na wafisadi”, alisema Rais Ruto.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending