News
Furaha Chengo:Sijaagizwa nijiondoe kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo Magarini
Mgombea wadhifa wa ubunge katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kupitia chama cha DCP Furaha Chengo Ngumbao almaarufu Kalama Wehu, amekana kupokea maagizo ya kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo eneo hilo la Magarini ulioratibiwa kufanyika mwezi Novemba 27, 2025.
Katika mahojiano kwenye kipindi cha Coco asubuhi, Kalama Wehu aliseme hajapokea maagizo yeyote ana iwapo hilo litatokea, ataendelea na harakati zake za kugombea wadhifa huo.
Matamshi ya Chengo yanajiri kufuatia madai kuwa mgombea huyo aliagizwa ajiondoe kwenye kinyang’anyiro hicho kutokana na kesi inayomkabili mahakamani.
Mwanaharakati huyo wa kisiasa alisema anaimani ya kuibuka na ushindi katika uchaguzi huo mdogo japo wapinzani wake wamekuwa wakitumia mbinu fiche za kuhujumu harakati zake za kuwania kiti hicho.
“Sijawahi kuitwa na mambo kama hayo na nikiitwa sinitakuwa nimeitwa? na uamuzi utakuwepo? wa kwamba mimi sishuki na nikishuka nitashuka na watu wa Magarini, yaani wanatafuta mbinu yeyote na walinitega kutoka kitambo, hii kushikwa na kufungwa vitu ambavyo havina hata kesi vimekuwepo kwa sababu wakiangalia watu mashinani wamewakataa”,alisema Chengo.
Wakati huo huo Chengo aliahidi kuboresha uchumi wa eneo hilo iwapo ataibuka na ushindi, kwa kuondoa ada za mashamba ili kuwapa nafasi wakaazi kujiendeleza kiuchumi kupitia kilimo.
“Kutoka mimi nizaliwe Magarini uchumi ulioko pale ni ule wa chumvi pekeyake ilihali tuko na nafasi ya kuwekeza viwanda vingi sana pale ndani ya Magarini, kuna sehemu zimefika umeme, zimefika barabara, zimefika maji, kumaanisha kwamba tukiweka viwanda vinaweza kufanya vizuri na wakaazi wapate ajira”,aliongeza mwanaharakati huyo.
Furaha Chengo alikamatwa kwa madai ya kuhusika katika maandamano ya kizazi cha Gen Z ya tarehe 25 mwezi Juni 2025, yaliyofanyika mjini Malindi na kusababisha vurugu zilizopelekea kuvunjwa kwa jengo la Al Noor, kunakopatikana makao makuu ya Ofisi za NSSF tawi la Malindi.
Uchaguzi huo mdogo unatarajiwa kuwa na ushindani makali baada ya vyama vya kisiasa kuwakabidhi vyeti wagombea wao waliotangaza nia ya kuwania wadhfa wa ubunge wa Magarini.
Katika uchaguzi huo mdogo, bendera ya chama cha ODM itapeperusha Harrison Garama Kombe anayelenga kutetea kiti chake baada ya ushindi wake kubatilishwa na Mahakama kuu.

Harrison Kombe anayegombea wadhfa wa ubunge Magarini kupitia chama cha ODM.
Chama cha Wiper kilimpa cheti Samuel Nzai kuwania wadhfa huo, huku chama cha UDA kikiwakilishwa na Stanley Karisa Kenga.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

