News
Gavana Sakaja aponea shoka la kutimuliwa mamlakani
Mchakato wa kumbandua mamlakani Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja pamoja na Naibu wake James Muchiri umekosa kuendelea baada ya Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kuingilia kati mchakato huo.
Hii ni baada ya Odinga pamoja na viongozi wakuu wa chama cha ODM na Wawakilishi wadi wa kaunti ya Nairobi kufanya kikao cha mazungumzo kwa masaa kadhaa na kuibuka na suluhisho la kusitishwa kwa mchakato huo.
Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho kilichoandaliwa jijini Nairobi, Mbunge wa Makadara George Aladwa alisema kikao hicho kimasikiliza lalama zote zilizoibuliwa na wawakilishi wadi hao dhidi ya Gavana Sakaja na kuafikia masuala kadhaa.
Aladwa alisema Gavana Sakaja amehimizwa kurekebisha masuala yalioibuliwa na Wawakilishi wadi hao sawa na kushirikiana naoi li kuhakikisha kaunti ya Nairobi inapiga hatua kimaendeleo na wananchi wa kaunti hiyo wananufaika.
Siku ya Jumatatu Septemba 1, 2025, Wawakilishi wadi hao wa Nairobi wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Kileleshwa Robert Alai, walisema Gavana Sakaja alishindwa kuwajibikia majukumu yake kama Gavana na kwamba hafai kushikilia wadhfa huo.
Wawakilishi wadi hao waliorodhesha malalamishi zaidi ya 20 dhidi ya Gavana Sakaja ikiwemo uongozi duni, ukiukaji wa Katiba, usimamizi duni wa jiji la Nairobi, kuporomoka kwa majengo kiholela, mirundiko ya taka katikati wa jiji, huduma duni za afya, miongoni mwa masuala mengine.
Wawakilishi wadi hao walisema wako na ushahidi wa kutosha dhidi ya Gavana Sakaja, wakishikilia kwamba Gavana huyo ameshindwa kusimamia jiji la Nairobi, wakipendekeza kutimuliwa Mamlakani pamoja na Naibu wake James Muchiri.
Itakumbukwa kwamba Wawakilishi wadi zaidi ya 100 walikuwa tayari wametia saini hoja ya kumbandua mamlakani Gavana Sakaja pamoja na Naibu wake James Muchiri kwa madai ya kushindwa kuwajibikia majukumu yao miongoni mwa hoja zengine zaidi ya 20 lakini hatua ya Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kuingilia kati suala hilo kulimnuru Gavana Sakaja.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wajumbe wa bunge la Seneti wazuru kaunti ya Kilifi
Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi na kupokelewa na Karani wa bunge hilo Michael Ngala.
Wajumbe hao wa sekta mbalimbali wa bunge la Seneti wakiongozwa na Daniel Chania, wametathmini masuala mbalimbali ya bunge la kaunti ya Kilifi kama lina uwezo wa kuandaa ziara ijayo ya Seneti mashinani.
Seneti Mashinani ilianzishwa chini ya kifungu cha 126 ibara ya kwanza ya Katiba ya Kenya ya mwaka 2010, kinachoruhusu kikao cha bunge lolote kufanyika mahali popote ndani ya taifa la Kenya na kuanza wakati wowote kitakapopangwa na bunge.
Malengo ya vikao hivyo katika kaunti ni pamoja na kuhamasisha umma kuhusu kazi za bunge na Seneti, kuimarisha ushiriki wa umma katika shughuli za Seneti kwenye ngazi ya kaunti sawa na kutoa hamasa kwa wananchi kwa lengo la kuhimiza ushiriki umma katika utawala.

Baadhi ya wajumbe wa bunge la Seneti chini ya mpango wa Seneti mashinani wamefanya ziara katika majengo ya bunge la kaunti ya Kilifi
Bunge la Seneti limeanza maandalizi ya vikao vitakavyofanyika nje ya Nairobi, ambavyo vinatarajiwa kufanyika mwezi Septemba 2026.
Kaunti ya Kilifi ni miongoni mwa kaunti zilizoteuliwa kuwa kati ya zile zitazoandaa vikao hivyo kwa ajali ya umma kuwa na uelewa zaidi kuhusu shughuli za bunge hilo.
Wajumbe hao walikuwa na malengo pia ya kubaini upatikanaji wa miundombinu na huduma muhimu ili kuiwezesha Seneti kufanya uamuzi.
Kaunti nyingine zilizowahi kuandaa Seneti Mashinani ni pamoja na kaunti ya Uasin Gishu mwaka 2018, ikifuatiwa na kaunti ya Kitui mwaka 2019, kaunti ya Turkana mwaka 2023 na kaunti ya Busia mwaka 2025.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Sakata ya mafuta yaathiri sekta ya uchukuzi nchini
Huenda watumizi wa magari ya uchukuzi wa umma, wahudumu wa tuktuk na bodaboda wakalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na changamoto za ukosefu wa mafuta nchini na kuathiri zaidi shughuli za uchukuzi.
Hatua hii imetakana na changamoto za uhaba wa mafuta nchini baada ya kuibuka kwa sataka ya uagizaji wa mafuta ghushi kupitia bandari ya Mombasa.
Kulingana na serikali kupitia Wizara ya Kawi, sakata hiyo ya shilingi bilioni 12 ilikuwa imelata tani elfu 60 za mafuta ya petroli kinyume cha sheria pamoja na mipango ya serikali ya uagizaji mafuta wa serikali kwa serikali yaani G to G.
Sakata hii imepelekea Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya kudhibiti kawi na bei za mafuta nchini EPRA Daniel Kiptoo, Katibu katika Idara ya petroli nchini Mohammed Liban na mkurugenzi wa Kampuni ya Kenya Pipeline Joe Sang kujiuzulu.
Kujiuluzu kwao kumetokana na kukamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI, kwa ushirikiano na Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC baada ya kutilia shaka zabuni iliyopewa kampuni binafsi ya One Petroleum Limited inayomilikwa na mfanyibiashara mashuhuri jijini Mombasa.

Wahudumu wa sekta ya bodaboda wakikabiliwa na changamoto za uhaba wa mafuta ya Petroli
Siku ya Jumanne, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandanyi alifanya kikao na wakurugenzi wa kampuni za mafuta nchini na kuagiza shehena ya mafuta katika bandari ya Mombasa kurejeshwa kwani serikali haitambua shehena hiyo.
“Wahusika wa sakata hiyo walikuwa na njama ya kuongeza bei ya mafuta nchini kwa shilingi 14 zaidi kwa lita wakitumia nafasi ya vita vinavyoendelea kati ya Iran na Marekani na Israel, hiyo hatuta kubali”, alisema Wandayi.
Hatua hiyo ilikuwa inalenga pia kukwepa mpango wa serikali wa uagizaji mafuta kutoka mataifa ya miliki za kiarabu wa serikali kwa serikali yaani G to Go, akisema wahusika wa sakata ya ufisadi ni lazima wachukuliwe hatua.
Itakumbukwa kwamba rais William Ruto hivi majuzi alidokeza kwamba wahusika wote wa sakata ya ufisadi kwenye sekta ya mafuta watachukuliwa hatua, akishililia kwamba serikali haitakubali ufisadi nchini, huku akikosa kuweka wazi hatma ya maafisa hao wakuu wa serikali.
“Hawa walaghai wa mambo ya mafuta watakipata, hawaweze kuhepa kwa sababu haiwezekani katika taifa letu la Kenya watu wanaone tuko na shida ya mashariki ya kati wanakuja kukoroga shida nyengine hapa Kenya, serikali itakabiliana kikamilifu na wafisadi”, alisema Rais Ruto.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

