Connect with us

News

Gavana Sakaja aponea shoka la kutimuliwa mamlakani

Published

on

Mchakato wa kumbandua mamlakani Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja pamoja na Naibu wake James Muchiri umekosa kuendelea baada ya Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kuingilia kati mchakato huo.

Hii ni baada ya Odinga pamoja na viongozi wakuu wa chama cha ODM na Wawakilishi wadi wa kaunti ya Nairobi kufanya kikao cha mazungumzo kwa masaa kadhaa na kuibuka na suluhisho la kusitishwa kwa mchakato huo.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho kilichoandaliwa jijini Nairobi, Mbunge wa Makadara George Aladwa alisema kikao hicho kimasikiliza lalama zote zilizoibuliwa na wawakilishi wadi hao dhidi ya Gavana Sakaja na kuafikia masuala kadhaa.

Aladwa alisema Gavana Sakaja amehimizwa kurekebisha masuala yalioibuliwa na Wawakilishi wadi hao sawa na kushirikiana naoi li kuhakikisha kaunti ya Nairobi inapiga hatua kimaendeleo na wananchi wa kaunti hiyo wananufaika.

Siku ya Jumatatu Septemba 1, 2025, Wawakilishi wadi hao wa Nairobi wakiongozwa na Mwakilishi wadi ya Kileleshwa Robert Alai, walisema Gavana Sakaja alishindwa kuwajibikia majukumu yake kama Gavana na kwamba hafai kushikilia wadhfa huo.

Wawakilishi wadi hao waliorodhesha malalamishi zaidi ya 20 dhidi ya Gavana Sakaja ikiwemo uongozi duni, ukiukaji wa Katiba, usimamizi duni wa jiji la Nairobi, kuporomoka kwa majengo kiholela, mirundiko ya taka katikati wa jiji, huduma duni za afya, miongoni mwa masuala mengine.

Wawakilishi wadi hao walisema wako na ushahidi wa kutosha dhidi ya Gavana Sakaja, wakishikilia kwamba Gavana huyo ameshindwa kusimamia jiji la Nairobi, wakipendekeza kutimuliwa Mamlakani pamoja na Naibu wake James Muchiri.

Itakumbukwa kwamba Wawakilishi wadi zaidi ya 100 walikuwa tayari wametia saini hoja ya kumbandua mamlakani Gavana Sakaja pamoja na Naibu wake James Muchiri kwa madai ya kushindwa kuwajibikia majukumu yao miongoni mwa hoja zengine zaidi ya 20 lakini hatua ya Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga kuingilia kati suala hilo kulimnuru Gavana Sakaja.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending