Connect with us

News

“Handshake” ya Rais Ruto na Gedion Moi

Published

on

Rais William Ruto amevunja kimya chake na kuweka wazi kuhusu mkutano wa faraja uliandaliwa kati yake na Mwenyekiti wa chama cha KANU Gedion Moi katika Ikulu ya Nairobi siku ya Jumanne.

Rais Ruto alisema masuala walioafikiana ni pamoja na Gedion Moi kujiunga na serikali jumuishi yaani Broad-based Government, akitetea hatua ya Gedion kujiondoa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo wa useneti, kaunti ya Baringo.

Akizungumza katika eneo la Kabarak kaunti ya Nakuru wakati wa mkutano na viongozi wa chama cha KANU, Rais Ruto alisema asilimia 90 ya wakenya wanamiliki nyumba, na kwamba ushirikiana wake na Gedion utasaidia kuafikia matakwa ya wakenya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha KANU, Gedion Moi alisema ushirikiano wa viongozi hao wawili unalenga kufanikisha malengo ya wananchi na kwamba hatua hiyo imemfanya kufanya maamuzi ya kujiondoa katika uchaguzi mdogo wa useneti wa Baringo.

Rais William Ruto na Mwenyekiti wa chama cha KANU katika mkutano wa wajumbe wa chama hicho eneo la Kabarak kaunti ya Nakuru

Hata hivyo wandani wa kisiasa wa viongozi hao wawili walisema ushirikiano wa Rais Ruto na Gedion Moi ni kuhakikisha familia ya Moi inapata ulinzi wa raslimali zao pamoja na masuala mengine ya ndani hasa maslahi ya kisiasa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending