Connect with us

News

“Handshake” ya Rais Ruto na Gedion Moi

Published

on

Rais William Ruto amevunja kimya chake na kuweka wazi kuhusu mkutano wa faraja uliandaliwa kati yake na Mwenyekiti wa chama cha KANU Gedion Moi katika Ikulu ya Nairobi siku ya Jumanne.

Rais Ruto alisema masuala walioafikiana ni pamoja na Gedion Moi kujiunga na serikali jumuishi yaani Broad-based Government, akitetea hatua ya Gedion kujiondoa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo wa useneti, kaunti ya Baringo.

Akizungumza katika eneo la Kabarak kaunti ya Nakuru wakati wa mkutano na viongozi wa chama cha KANU, Rais Ruto alisema asilimia 90 ya wakenya wanamiliki nyumba, na kwamba ushirikiana wake na Gedion utasaidia kuafikia matakwa ya wakenya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha KANU, Gedion Moi alisema ushirikiano wa viongozi hao wawili unalenga kufanikisha malengo ya wananchi na kwamba hatua hiyo imemfanya kufanya maamuzi ya kujiondoa katika uchaguzi mdogo wa useneti wa Baringo.

Rais William Ruto na Mwenyekiti wa chama cha KANU katika mkutano wa wajumbe wa chama hicho eneo la Kabarak kaunti ya Nakuru

Hata hivyo wandani wa kisiasa wa viongozi hao wawili walisema ushirikiano wa Rais Ruto na Gedion Moi ni kuhakikisha familia ya Moi inapata ulinzi wa raslimali zao pamoja na masuala mengine ya ndani hasa maslahi ya kisiasa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending