Connect with us

News

Hofu ya Ongezeko la HIV

Published

on

Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na virusi vya UKIMWI, UNAIDS, limesema huenda kukawa na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi milioni 6 na vifo milioni 4 vinavyohusiana na ukimwi kufikia mwaka 2029.

Hii ni kutokana na kupunguzwa kwa fedha za misaada ya kiafya kutoka Shirika la Marekani, USAIDS.

Kulingana na takwimu, taifa la Afrika kusini ndio taifa lenye idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ulimwenguni lakini pia nchi inayoongoza katika utafiti wa virusi vya ukimwi ulimwenguni.

Miongoni mwa mataifa mengine, Afrika kusini pia imekuwa nchi ambayo pia ilikuwa ni mpokeaji mkubwa wa fedha za UKIMWI kutoka Marekani hadi Machi mwaka huu, wakati utawala wa Rais Trump ulipotangaza kufungwa kwa Shirika la USAID.

Mwezi uliopita vyuo vikuu vya juu vya Afrika Kusini viliomba serikali madola ya mamilioni ili kuendelea na utafiti huu ambao baadhi umesitishwa kwa sababu ya kupunguzwa kwa fedha na Marekani.

Pesa hii ilisaidia nchi hiyo kupunguza kiwango chake cha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya asilimia 60 tangu kilele chake mnamo 2000.

Siku ya Jumatano tarehe 9 Julai 2025, serikali ya Afrika Kusini na wafadhili wa kimataifa waliahidi karibu dola milioni 54 ili kukabili palipo na mapungufu.

Mwaka jana Marekani ilitumia mara nane ya kiwango hicho kwa ufadhili wa Virusi Vya Ukimwi Afrika Kusini kiwango hiki hakitatosha kutimiza hitaji lililopo.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending