News
Hofu ya Ongezeko la HIV
Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na virusi vya UKIMWI, UNAIDS, limesema huenda kukawa na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi milioni 6 na vifo milioni 4 vinavyohusiana na ukimwi kufikia mwaka 2029.
Hii ni kutokana na kupunguzwa kwa fedha za misaada ya kiafya kutoka Shirika la Marekani, USAIDS.
Kulingana na takwimu, taifa la Afrika kusini ndio taifa lenye idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ulimwenguni lakini pia nchi inayoongoza katika utafiti wa virusi vya ukimwi ulimwenguni.
Miongoni mwa mataifa mengine, Afrika kusini pia imekuwa nchi ambayo pia ilikuwa ni mpokeaji mkubwa wa fedha za UKIMWI kutoka Marekani hadi Machi mwaka huu, wakati utawala wa Rais Trump ulipotangaza kufungwa kwa Shirika la USAID.
Mwezi uliopita vyuo vikuu vya juu vya Afrika Kusini viliomba serikali madola ya mamilioni ili kuendelea na utafiti huu ambao baadhi umesitishwa kwa sababu ya kupunguzwa kwa fedha na Marekani.
Pesa hii ilisaidia nchi hiyo kupunguza kiwango chake cha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya asilimia 60 tangu kilele chake mnamo 2000.
Siku ya Jumatano tarehe 9 Julai 2025, serikali ya Afrika Kusini na wafadhili wa kimataifa waliahidi karibu dola milioni 54 ili kukabili palipo na mapungufu.
Mwaka jana Marekani ilitumia mara nane ya kiwango hicho kwa ufadhili wa Virusi Vya Ukimwi Afrika Kusini kiwango hiki hakitatosha kutimiza hitaji lililopo.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

