Connect with us

Sports

Ligi ya kaunti ya Kilifi kungoa nanga Machi 21 asema mwenyekiti Dickson Angore

Published

on

Ligi Kuu ya Kaunti ya Kilifi chini ya Shirikisho la Soka nchini (FKF) inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 21 Machi mwaka huu. Uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki uliowakutanisha maafisa wa vilabu pamoja na viongozi wa tawi la FKF Kilifi.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Mwenyekiti wa FKF tawi la Kilifi, Dickson Angore, alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika ili kuhakikisha msimu huu unafanyika kwa mafanikio.

“Tumefanya mkutano na vilabu na matumaini yetu ni kwamba ligi itaanza mwezi ujao, Mungu akipenda, kwani tayari imechelewa kuanza. Lengo letu ni kuhakikisha kila kitu kiko sawa kabla ya kipenga cha kwanza,” alisema Angore.

Katika kikao maalum kilichowahusisha wakufunzi na wasimamizi wa vilabu mjini Kilifi, ilikubaliwa kuwa baada ya makubaliano kuhusu ada za usajili na ushiriki, pamoja na vilabu kutimiza wajibu wao wa kifedha, ligi hiyo itafunguliwa rasmi.

“Tunatarajia vilabu vitawajibika kulipa ada kwa wakati ili tuanze mchakato wa usajili na utengenezaji wa kadi za wachezaji, jambo litakalowezesha ligi kuanza bila vikwazo,” aliongeza mwenyekiti huyo.

Angore pia alithibitisha kuwa kozi za ukocha zitaanza ndani ya wiki mbili zijazo, akitoa shukrani kwa Wizara ya Michezo ya Kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano wake na shirikisho hilo.

“Tumewasilisha mipango yetu kwa kaunti na makocha wako tayari. Tunatarajia ndani ya wiki mbili zijazo mafunzo hayo yaanze rasmi. Aidha, tunaendelea na mazungumzo na ofisi ya kitaifa ili tuongeze darasa lingine kwa kuwa lililopo halitoshelezi mahitaji,” alisema.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa FKF tawi la Kilifi, Odak Onyango, alisisitiza umuhimu wa nidhamu na uwajibikaji kutoka kwa vilabu, hasa katika kufuata ratiba ya mechi.

“Ratiba itatolewa mara tu vilabu vitakapokamilisha malipo ya ada ya ushiriki. Naomba vilabu vizingatie ratiba kikamilifu ili kuepusha sababu za kuahirisha mechi tena,” alieleza Onyango.

Naye Mwakilishi wa Wanawake wa FKF Kilifi, Elizabeth Hinzano, alieleza masikitiko yake kuhusu kushuka kwa kiwango cha soka la wanawake kaunti humo, akiahidi kuchukua hatua za kulifufua.

“Inasikitisha kuona soka la wanawake likidorora kwa sababu wengi hawajawa tayari kujihusisha nalo. Hata hivyo, nina imani kwamba chini ya uongozi wangu tutaleta mwamko mpya. Ninalenga kuwawezesha wasichana na kuwasaidia kujenga taaluma katika ukocha na uongozi wa soka,” alisema Hinzano.

Jumla ya vilabu 74 vilihudhuria mkutano huo, vikionesha nia ya kushiriki katika Ligi Kuu ya Kaunti ya Kilifi msimu huu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Sekta ya Baiskeli kuimarisha matumizi ya usafiri endelevu

Published

on

By

Mamia ya waendesha baiskeli walijumuika na viongozi wa kaunti ya Mombasa pamoja na wadau wa sekta ya usafiri walijitokeza kuonyesha dhamira ya kuendeleza miundombinu salama ya waendesha baiskeli na kuhimiza matumizi ya usafiri endelevu.

Waendeshajio hao wa baiskeli walionyesha dhamira hiyo kufuatia kuendelea kushuhudia maendeleo makubwa katika ujenzi wa njia maalum za waendesha baiskeli, hatua inayolenga kupunguza msongamano wa magari, kuboresha afya ya wananchi na kupunguza uzalishaji wa hewa kaa.

Mkurugenzi Mkuu wa EBee Africa, Maarten Fonteijn, alisema mpango huo pia uliambatana na kusherehekea kukamilika kwa awamu ya kwanza ya njia ya waendesha baiskeli katika kaunti hiyo.

Alibainisha kuwa matumizi ya baiskeli ni suluhisho mojawapo la changamoto ya msongamano wa magari mjini Mombasa kwani yanawawezesha wananchi kufika maeneo yao kwa haraka huku wakiboresha afya zao.

“Tunafurahia kukamilika Kwa njia ya baiskeli itasaidia pakubwa pia katika kupunguza msongamani wa magari”

Kwa upande wake, mkurugenzi wa Kanda wa ITDP Africa Claire Birungi alisema idadi kubwa ya watu waliojitokeza kushiriki hafla hiyo ni ishara kwamba wananchi wamekubali matumizi ya baiskeli na sasa kilichobaki ni kuimarisha miundombinu salama ya waendesha baiskeli.

Aliongeza kuwa ujenzi wa njia ya baiskeli katika Barabara ya Links tayari umeanza, ambapo takribani kilomita nne zimejengwa na mipango ipo ya kuipanua hadi kilomita nane.

“ Zaidi ya waendesha baiskeli 200 wamejitokeza kuunga mkono shughuli hii. Tunahitaji kuendelea kuwekeza katika miundombinu salama ya baiskeli inayounganishwa na mifumo mingine ya usafiri wa umma,”

Wadau hao walieleza kuwa miundombinu bora ya baiskeli itasaidia watoto kusafiri kwa usalama, kukuza biashara kwa kurahisisha ufikiaji wa wateja na kuwapa wananchi njia nafuu na salama ya usafiri.

Kwa upande wake meneja wa programu Global Designing Cities Initiative, Regatu Solomon alisema Mombasa ni miongoni mwa miji kumi duniani iliyochaguliwa kati ya miji 275 kufaidika na mpango wa Bloomberg Initiative for Cycling Infrastructure (BICI), unaosaidia miji kujenga miundombinu salama na jumuishi ya waendesha baiskeli.

“Tunatoa msaada wa kiufundi na kifedha ili kusaidia Mombasa kutekeleza miundombinu salama ya waendesha baiskeli kwa manufaa ya watumiaji wote wa barabara,” alisema.

Nae Naibu Gavana wa Kaunti ya Mombasa, Francis Thoya, alisema matumizi ya baiskeli yanazidi kuwa mtindo wa maisha na suluhisho la changamoto za usafiri zinazokabili kaunti hiyo.

Aliweka wazi kuwa serikali ya kaunti kwa ushirikiano na wadau mbalimbali tayari imeanza kupanua miundombinu ya baiskeli kutoka Barabara ya Links kuelekea katikati ya jiji ili kuwahamasisha wananchi kutumia zaidi usafiri huo.

Zaidi ya waendesha baiskeli 200 wajitokeza kuunga mkono shughuli usafiri endelevu wa baiskeli Mombasa

Thoya pia alisisitiza umuhimu wa baiskeli katika kulinda mazingira kwa kupunguza uzalishaji wa hewa chafu kutoka kwa magari.

“Mombasa ni kaunti ndogo zaidi nchini Kenya lakini inaendelea kukua kwa kasi. Eneo ni finyu na msongamano wa magari unaongezeka kila siku. Ni wakati wa wananchi kuanza kufikiria njia mbadala za usafiri,ambayo pia itasaidia kulinda mazingira yetu,”

Mombasa inaelekea kuwa miongoni mwa miji inayoongoza katika kuhamasisha matumizi ya baiskeli kama njia salama, nafuu na endelevu ya usafiri.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Sports

Bingwa wa Afrika mbio za mita 100 mkenya Ferdinand Omanyala azidi kuthibitisha ubora wake mbio Botswana Golden Grand Prix akimaliza wa pili na sekunde 9.95

Published

on

By

Mwanariadha mwenye kasi zaidi barani Afrika, Ferdinand Omanyala, amethibitisha kurejea kwake katika kiwango cha juu kwa mbio za kuvutia za sekunde 9.95 kwenye mashindano ya Botswana Golden Grand Prix yaliyofanyika Jumapili, Aprili 26 jijini Gaborone.

Katika fainali ya wanaume ya mita 100 iliyokuwa na ushindani mkali, Mkanada Jerome Blake alishinda kwa sekunde 9.93, huku mwenzake Andre De Grasse na Omanyala wakitumia sekunde 9.95 katika ushindani wa karibu sana. Ingawa awali ilionekana kama nafasi ya pili iligawanywa, matokeo rasmi yalimweka Omanyala katika nafasi ya tatu kwa tofauti ndogo sana.

Licha ya nafasi hiyo, matokeo hayo yaliashiria mbio ya tatu mfululizo kwa Omanyala kukimbia chini ya sekunde 10 ndani ya siku saba tu, na kukamilisha kurejea kwa nguvu kwa mshikiliaji wa rekodi ya Afrika. Mkenya huyo alianza mfululizo huo kwa ushindi wa sekunde 9.98 katika Addis Ababa Grand Prix Aprili 18, kabla ya kuwapa mashabiki wa nyumbani burudani kwa ushindi wa sekunde 9.96 katika mashindano ya Kip Keino Classic jijini Nairobi Aprili 24.

Mfululizo huu wa matokeo unaashiria kurejea kwa nguvu kwa Omanyala baada ya msimu mgumu wa 2025 uliokumbwa na majeraha na kutokuwepo kwa uthabiti, ambapo alishindwa kushuka chini ya kiwango muhimu cha sekunde 10.

Sasa macho yanaelekezwa kwenye World Athletics Relays zitakazofanyika Mei 2–3, pia jijini Gaborone, ambapo Omanyala anatarajiwa kuiongoza timu ya Kenya katika mbio za kupokezana vijiti za 4x100m. Mashindano hayo yatakuwa hatua muhimu kuelekea kufuzu kwa michuano ya Ultimate Championship itakayofunga msimu.

Kwa kuzingatia mashindano yajayo ya Continental Tour Gold na michuano mikubwa kama Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Glasgow, kurejea huku kwa kasi kwa Omanyala kumekuja wakati muafaka anapojenga upya kasi yake dhidi ya wanariadha bora duniani.

Continue Reading

Trending