Connect with us

News

Mahakama ya Shanzu yaagiza kuzuiliwa kwa washukiwa wa mihadarati ya Methamphetamine

Published

on

Mahakama ya Shanzu imeagiza washukiwa sita wa ulanguzi wa dawa ya kulevya aina ya Methamphetamine zenye thamani ya shilingi bilioni 8.2 kusalia korokoroni kwa siku 30 ili kufanikisha uchunguzi.

Hakimu mkuu wa Mahakama ya Shanzu Anthony Mwicigi aliagiza washukiwa hao kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Bandari na kupewa huduma muhimu za matibabu.

Mwicigi ameagiza pia 6 hao kurejeshwa Mahakamani mnamo tarehe 14 mwezi Novemba ambapo ripoti ya uchunguzi wa kiafya itatolewa na kisha kesi hiyo kusikizwa mnamo tarehe 27 mwezi huo wa Novemba.

Afisa mkuu wa upelelezi katika kesi hiyo Shadrack Kemei aliambia Mahakama kwamba kati ya washukiwa hao 6 waliokamatwa, wanne pekee ndio raia wa Iran huku wawili wakiwa bado hawajatambuliwa uraia wao.

Kemei alisema shehena ya dawa za kulevya pamoja na vifaa vya mawasiliano vilivyokamatwa vitahitaji kufanyiwa uchunguzi kwenye maabara ya Serikali ili kubaini uhalisia wa dawa hizo.

“Kati ya washukiwa hawa 6 waliokamatwa, wanne pekee ndio raia wa Iran na wawili bado hawajatambuliwa uraia wao na bado tunafanya uchunguzi kuhusu dawa hizo za kulevya kwani shehena iliyokuwa na dawa hizo ni kubwa sana lakini bado tunafuatilia kubaini mmiliki halisi wa shehena hiyo”, alisema Kemei.

Wakati huo huo Kemei aliomba Mahakama kutowapa dhamana washukiwa hao, akisema ni tishio kwa usafiri kwani huenda wakahitilafiana na uchunguzi, huku akidokeza kuwa huenda 6 hao wanajumuisha mtandao mkubwa wa walanguzi dawa za kulevya.

Kauli yake ilisisitizwa zaidi ya kiongozi wa mashtaka Anthony Musyoka ambaye ameiomba Mahakama kuendelea kuwazuia sita hao kwa siku zaidi ili kukamilisha uchunguzi na kubaini iwapo dawa hizo zilikuwa zinaelekezwa kwa nani.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending