News
Watu 12 wahofiwa kufariki baada ya ndege kuanguka Kwale
Watu 12 wanahofiwa kufariki baada ya ndege ndogo ya utalii kuanguka katika eneo la Tsimba gatuzi dogo la Matuga kaunti ya Kwale.
Ndege hiyo ilikuwa imetokea eneo la Diani kuelekea Kichwa Tembo kwa shughuli za kiutalii katika eneo la Masai Mara kabla ya kuanguka na kuchomeka.
Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa anga nchini KCAA, Emile Arao, alisema ndege hiyo ndogo yenye nambari ya usajili 5Y-CCA ilikuwa na abiria 12 wenye asili ya Ugerumani ambao walikuwa wameabiri ndege hiyo.
Arao alisema tayari maafisa wa usafari wa angani wameanzisha uchunguzi ili kubaini kiini cha ajali hiyo kwani hata mabaki ya ndege hiyo yalichomeka.


Taarifa ya Mamlaka ya usafiri wa anga nchini KCAA kuhusu kuanguka kwa ndege ya 5Y-CCA
Ajali hiyo ya ndege imetokea miezi kadhaa baada ya ndege ndogo ya Wanajeshi kuanguka katika kaunti hiyo ya Kwale kutokana na changamoto za kimitambo.
Hii sio mara ya kwanza mikasa ya ndege kuanguka kushuhudiwa katika ukanda wa Pwani ambapo ndege yengine ndogo ilikuwa katika mafunzo ya marubani ilikumbwa na hitilafu za kimitambo na kuanguka katika eneo la Kwa Chocha mjini Malindi.
Ajali hiyo ya Malindi ilisababisha vifo vya watu wawili ingawa changamoto kubwa ni kwamba hakujakuwa na taarifa zozote kuhusu ripoti ya kilichosababisha ajali hiyo na hata fidia kwa familia zilizopoteza wapendwa wao.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

