Connect with us

News

Mahakama ya Shanzu yaagiza kuzuiliwa kwa washukiwa wa mihadarati ya Methamphetamine

Published

on

Mahakama ya Shanzu imeagiza washukiwa sita wa ulanguzi wa dawa ya kulevya aina ya Methamphetamine zenye thamani ya shilingi bilioni 8.2 kusalia korokoroni kwa siku 30 ili kufanikisha uchunguzi.

Hakimu mkuu wa Mahakama ya Shanzu Anthony Mwicigi aliagiza washukiwa hao kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Bandari na kupewa huduma muhimu za matibabu.

Mwicigi ameagiza pia 6 hao kurejeshwa Mahakamani mnamo tarehe 14 mwezi Novemba ambapo ripoti ya uchunguzi wa kiafya itatolewa na kisha kesi hiyo kusikizwa mnamo tarehe 27 mwezi huo wa Novemba.

Afisa mkuu wa upelelezi katika kesi hiyo Shadrack Kemei aliambia Mahakama kwamba kati ya washukiwa hao 6 waliokamatwa, wanne pekee ndio raia wa Iran huku wawili wakiwa bado hawajatambuliwa uraia wao.

Kemei alisema shehena ya dawa za kulevya pamoja na vifaa vya mawasiliano vilivyokamatwa vitahitaji kufanyiwa uchunguzi kwenye maabara ya Serikali ili kubaini uhalisia wa dawa hizo.

“Kati ya washukiwa hawa 6 waliokamatwa, wanne pekee ndio raia wa Iran na wawili bado hawajatambuliwa uraia wao na bado tunafanya uchunguzi kuhusu dawa hizo za kulevya kwani shehena iliyokuwa na dawa hizo ni kubwa sana lakini bado tunafuatilia kubaini mmiliki halisi wa shehena hiyo”, alisema Kemei.

Wakati huo huo Kemei aliomba Mahakama kutowapa dhamana washukiwa hao, akisema ni tishio kwa usafiri kwani huenda wakahitilafiana na uchunguzi, huku akidokeza kuwa huenda 6 hao wanajumuisha mtandao mkubwa wa walanguzi dawa za kulevya.

Kauli yake ilisisitizwa zaidi ya kiongozi wa mashtaka Anthony Musyoka ambaye ameiomba Mahakama kuendelea kuwazuia sita hao kwa siku zaidi ili kukamilisha uchunguzi na kubaini iwapo dawa hizo zilikuwa zinaelekezwa kwa nani.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending