Connect with us

News

Miezi 11 Mochari: Hatimaye Mary Mutisya azikwa Tezo-Kilifi

Published

on

Kijiji cha Tezo eneo bunge la Kilifi Kazkazini kaunti ya Kilifi hali ilikuwa tofauti kwa familia ya Marehemu Mary Mutisya baada ya kuzuka mvutano wa kifamilia na kusababisha marehemu kusalia kwenye makafani ya hospitali kuu ya rufaa ya Kilifi kwa zaidi ya miezi 11.
Familia hiyo ilidai kwamba ilikuwa ikihangaishwa shangazi wao kutokana na umiliki wa ardhi wanaoishi ya zaidi ya ekari 24 katika kijiji hicho ambayo waliachiwa na baba yao ambaye kwa sasa ni marehemu pia.
Kulingana na familia hiyo ikiongozwa na Morgan Mwamuye, tangu kifo cha mamake mzazi mwezi Aprili 15, 2025 juhudi za kumzika zimekuwa zikgonga mwamba kutokana na shangazi zao kuzuia mazishi hayo kupitia kesi Mahakamani.

Familia yaomboleza kifo cha Mary alifariki tangu mwezi Aprili 15, 2025 na kusalia Mochari kwa kipindi cha miezi 11

Mwamunye aliasema licha ya kuchimba kaburi la mama yao, kuburi hilo lilifunikwa kutokana na agizo la Mahakama baada ya shangazi wa vijana hao kuwasilisha kesi Mahakamani, kwa misingi kwamba ardhi hiyo ni mali ya familia kuu na wala sio ya watoto wa marehemu, mvutano ambao ulidumu kwa muda mrefu.
“Sisi tumeishi kwa ardhi hii tangu tuko wadogo na hii nyumba hapa ilijengwa na kakangu mkubwa na akamuhamisha mama hapo na hatujakuwa na shida na shangazi zetu lakini sasa tunashangaa hawataki tumzike mama na hii shamba alitengeneza mama na kupanda miti na miembe hata minazi lakini leo tunahangishwa na shangazi zetu ni haki kweli?”, alisema Morgan mtoto wa Marehemu.

Mwili wa Marehemu Mary Mutisya hatimaye wazikwa kijiji cha Tezo, Kilifi

Morgan alisema kwamba kifo cha mamake kilikuwa cha kutatanisha kwani aliugua kwa muda mfupi na mguu wake ulikuwa umevimba na kutokwa maji kila mara hali iliyopelekea kifo chake. Licha ya kuwa na ufahamu wa kilichokuwa kikiendelea mamake mzazi hakupata msaada wowote.
Kwa upande wake, Raymond Mwamuye ambaye pia ni mtoto wa Marehemu alisema licha ya kuomba kupewa ruhusu kumzika mama yao bado ilikuwa changamoto kwani waliwahi kuchimba kaburi kwa mara tatu bila ya kupata idhini ya kumzika mama yao kwani maafisa wa usalama walikuwa wakilinda eneo hilo.
Aidha alisema shangazi zake ndio waliokuwa mstari wa mbele kuwapokonya ardhi yao na hata kuzuia familia yao kumzika mama yao, wakilenga kuuza ardhi hiyo.
Mzee Chai Anderson ambaye ni jirani wa familia hiyo ya Marehemu alisema haki ya familia ya marehemu inafaa kuzingatiwa na wala sio kuhangaisha kila mara akipendekeza serikali na viongozi kuingilia kati suala hilo kuinusuru familia hii.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi kutumia nguvu kukabiliana na wahalifu

Published

on

By

Huenda maafisa wa polisi wakutumia nguvu kupita kiasi katika kukabiliana na wahalifu ama wale wanaolenga kuzua vurugu na fujo mashinani.

Idara ya usalama nchini imesisitiza kwamba itakabiliana kikamilifu na magenge ya kihalifu ambayo yanaendeleza uhalifu mashinani na kutatiza shughuli za kibiashara, uchumi na usalama wa taifa.

Idara hiyo ilisema tayari imebaini magenge ya kihalifu ambayo yanatatiza usalama wa wananchi, huku wazazi wakilaumiwa kwa kuwatetea watoto wao licha ya kufahamu kwa tabia hiyo inazidi kuhatarisha maisha ya jamii mashinani.

Idara hiyo, ililalamikia kukithiri kwa utovu wa usalama hasa kaunti za Kwale, Mombasa na Lamu katika ukanda wa Pwani, kutokana na vijana wengi kuzama katika uraibu wa Mihadarati na ukosefu wa kazi, hatua iliyopelekea baadhi ya vijana kujiunga na magenge ya mapanga.

Kauli hiyo ya idara ya usalama ilijiri siku moja tu baada ya Kamanda wa Polisi kanda ya Pwani Ali Nuno, kuagiza maafisa wa polisi kuwapiga risasi magenge ya kihalifu ya vipanga kwa kutatiza usalama.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 umewasilishwa bungeni

Published

on

By

Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 na sheria za uchaguzi umewasilishwa katika bunge la Seneti.

Mswada huo unalenga kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba cha 99 na 193 pamoja na sheria za uchaguzi sehemu ya 24 na 25 ili kuwepo na uwazi kwa magavana wanaolenga kuwania nyadhfa za uongozi baada ya kukamilisha mihula yao.

Mswada huo uliowasilishwa na Seneta wa Kirinyaga James Murango unalenga pia kuzuia magavana waliomaliza mihula yao ya uongozi kutowania nyadhfa za useneta, ubunge ama uwakilishi wadi, kwani inakuwa vingumu kuchunguzwa.

Kuwasilishwa kwa mswada huo bungeni kufuatia hali magavana kuwania wadhfa wa useneta baada ya kukamilisha mihula yao ya uongozi hali ambayo imeleta sintofahamu ya kiuongozi, ikiashiria tamaa za uongozi na njama ya kuhitilafiana na ufuatiliaji wa matumizi ya raslimali za umma.

Seneta Murango alisema katika utekelezaji wa majukumu yao, magavana hulazimika kuwajibika mbele ya mabunge ya kaunti na Seneti kuhusu matumizi ya kifedha na kiutawala.

Wakati huo huo alidokeza kwamba iwapo mswada huo utapishwa na kuwa sheria utasaidia kufutilia usimamizi wa raslimali za kaunti na matumizi ya fedha kwani utazuia magavana kuhitilafiana na uchunguzi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending