Connect with us

News

Miezi 11 Mochari: Hatimaye Mary Mutisya azikwa Tezo-Kilifi

Published

on

Kijiji cha Tezo eneo bunge la Kilifi Kazkazini kaunti ya Kilifi hali ilikuwa tofauti kwa familia ya Marehemu Mary Mutisya baada ya kuzuka mvutano wa kifamilia na kusababisha marehemu kusalia kwenye makafani ya hospitali kuu ya rufaa ya Kilifi kwa zaidi ya miezi 11.
Familia hiyo ilidai kwamba ilikuwa ikihangaishwa shangazi wao kutokana na umiliki wa ardhi wanaoishi ya zaidi ya ekari 24 katika kijiji hicho ambayo waliachiwa na baba yao ambaye kwa sasa ni marehemu pia.
Kulingana na familia hiyo ikiongozwa na Morgan Mwamuye, tangu kifo cha mamake mzazi mwezi Aprili 15, 2025 juhudi za kumzika zimekuwa zikgonga mwamba kutokana na shangazi zao kuzuia mazishi hayo kupitia kesi Mahakamani.

Familia yaomboleza kifo cha Mary alifariki tangu mwezi Aprili 15, 2025 na kusalia Mochari kwa kipindi cha miezi 11

Mwamunye aliasema licha ya kuchimba kaburi la mama yao, kuburi hilo lilifunikwa kutokana na agizo la Mahakama baada ya shangazi wa vijana hao kuwasilisha kesi Mahakamani, kwa misingi kwamba ardhi hiyo ni mali ya familia kuu na wala sio ya watoto wa marehemu, mvutano ambao ulidumu kwa muda mrefu.
“Sisi tumeishi kwa ardhi hii tangu tuko wadogo na hii nyumba hapa ilijengwa na kakangu mkubwa na akamuhamisha mama hapo na hatujakuwa na shida na shangazi zetu lakini sasa tunashangaa hawataki tumzike mama na hii shamba alitengeneza mama na kupanda miti na miembe hata minazi lakini leo tunahangishwa na shangazi zetu ni haki kweli?”, alisema Morgan mtoto wa Marehemu.

Mwili wa Marehemu Mary Mutisya hatimaye wazikwa kijiji cha Tezo, Kilifi

Morgan alisema kwamba kifo cha mamake kilikuwa cha kutatanisha kwani aliugua kwa muda mfupi na mguu wake ulikuwa umevimba na kutokwa maji kila mara hali iliyopelekea kifo chake. Licha ya kuwa na ufahamu wa kilichokuwa kikiendelea mamake mzazi hakupata msaada wowote.
Kwa upande wake, Raymond Mwamuye ambaye pia ni mtoto wa Marehemu alisema licha ya kuomba kupewa ruhusu kumzika mama yao bado ilikuwa changamoto kwani waliwahi kuchimba kaburi kwa mara tatu bila ya kupata idhini ya kumzika mama yao kwani maafisa wa usalama walikuwa wakilinda eneo hilo.
Aidha alisema shangazi zake ndio waliokuwa mstari wa mbele kuwapokonya ardhi yao na hata kuzuia familia yao kumzika mama yao, wakilenga kuuza ardhi hiyo.
Mzee Chai Anderson ambaye ni jirani wa familia hiyo ya Marehemu alisema haki ya familia ya marehemu inafaa kuzingatiwa na wala sio kuhangaisha kila mara akipendekeza serikali na viongozi kuingilia kati suala hilo kuinusuru familia hii.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending