Connect with us

News

Mudavadi apinga ripoti ya kikosi maalum cha Kenya nchini Haiti kuhusika na ubakaji

Published

on

Serikali imepinga ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu tuhuma za ubakaji dhidi ya maafisa wake wanaohudumu nchini Haiti chini ya Ujumbe wa kimataifa wa usaidizi wa usalama wa kimataifa.

Katika barua iliyotumwa kwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutteres tarehe 7 Aprili, Waziri wa masuala ya kigeni wa Kenya Musalia Mudavadi alielezea wasiwasi wake kuhusu madai ya unyanyasaji wa kingono na dhuluma ambayo yaliripotiwa Agosti 2025.

Mudavadi alisema madai hayo yalichunguzwa mara moja kupitia Bodi ya uchunguzi na kupatikana kuwa hayana uthibitisho kwani hakukuwa na malalamishi yaliyowasilishwa kwa mamlaka yoyote na kwamba matokeo yaliwekwa wazi na mashirika ya Haiti na Umoja wa Mataifa hayakuwa na uthibitisho.

Mudavadi aliongeza kuwa wafanyakazi wa MSS walifuata kikamilifu mifumo yote ya uendeshaji na kwamba hakuna ripoti zilizobainisha utovu wa nidhamu.

Ripoti ya Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi Februari na kuwekwa hadharani mwezi Aprili inaeleza kwamba maafisa chini ya ujumbe unaoongozwa na Kenya nchini Haiti walihusishwa katika visa vinne vya unyanyasaji wa kingono, kisa kimoja kikihusisha mtoto wa miaka 12.

Ripoti hiyo inasema madai hayo yalithibitishwa na uchunguzi uliofanywa na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa. Kulingana na Umoja wa Mataifa madai hayo yanachunguzwa. Haijabainika iwapo maafisa hao ni raia wa Kenya.

Ujumbe unaoongozwa na Kenya, uliotumwa Haiti mwaka 2024 kusaidia kukabiliana na ghasia za magenge, kufuatia idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, sasa nafasi yake imechukuliwa na Kikosi cha Kukakabiliana na Magenge.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending