Connect with us

News

Mudavadi apinga ripoti ya kikosi maalum cha Kenya nchini Haiti kuhusika na ubakaji

Published

on

Serikali imepinga ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu tuhuma za ubakaji dhidi ya maafisa wake wanaohudumu nchini Haiti chini ya Ujumbe wa kimataifa wa usaidizi wa usalama wa kimataifa.

Katika barua iliyotumwa kwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Gutteres tarehe 7 Aprili, Waziri wa masuala ya kigeni wa Kenya Musalia Mudavadi alielezea wasiwasi wake kuhusu madai ya unyanyasaji wa kingono na dhuluma ambayo yaliripotiwa Agosti 2025.

Mudavadi alisema madai hayo yalichunguzwa mara moja kupitia Bodi ya uchunguzi na kupatikana kuwa hayana uthibitisho kwani hakukuwa na malalamishi yaliyowasilishwa kwa mamlaka yoyote na kwamba matokeo yaliwekwa wazi na mashirika ya Haiti na Umoja wa Mataifa hayakuwa na uthibitisho.

Mudavadi aliongeza kuwa wafanyakazi wa MSS walifuata kikamilifu mifumo yote ya uendeshaji na kwamba hakuna ripoti zilizobainisha utovu wa nidhamu.

Ripoti ya Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi Februari na kuwekwa hadharani mwezi Aprili inaeleza kwamba maafisa chini ya ujumbe unaoongozwa na Kenya nchini Haiti walihusishwa katika visa vinne vya unyanyasaji wa kingono, kisa kimoja kikihusisha mtoto wa miaka 12.

Ripoti hiyo inasema madai hayo yalithibitishwa na uchunguzi uliofanywa na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa. Kulingana na Umoja wa Mataifa madai hayo yanachunguzwa. Haijabainika iwapo maafisa hao ni raia wa Kenya.

Ujumbe unaoongozwa na Kenya, uliotumwa Haiti mwaka 2024 kusaidia kukabiliana na ghasia za magenge, kufuatia idhini ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, sasa nafasi yake imechukuliwa na Kikosi cha Kukakabiliana na Magenge.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending