News
Shambulio la Osotsi lazua wasiwasi kwa upinzani
Seneta wa Vihiga Godfrey Ososti anaendelea kupokea matibabu katika Hospitali ya Karen jijini Nairobi baada ya kusafirishwa kwa ndege jana Jumatano April 8 2026 kutoka mjini Kisumu, siku moja tu baada ya Naibu Kinara huyo wa Chama cha ODM, kuvamiwa na kundi la vijana waliojihami kwa silaha hatari mjini Kisumu.
Viongozi mbali mbali hasa kutoka upande wa upinzani nchini Kenya, wamekuwa wakitoa kauli kali za kushtumu shambulio hilo wakihoji nia na dhamira ya shambulio hilo.
Osotsi ni miongoni mwa Viongozi wanaoasi Chama cha Odm katika mrengo wa Linda Mwananchi, wakiongozwa na Seneta wa Nairobi ambaye pia ni Katibu wa chama hicho Edwin Sifuna.
Wakiongozwa na Knara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka, walisema shambulio hilo dhidi ya seneta Osotsi huenda ni njama na vitisho kwa kusudi la kuzua uhasama baina ya jamii mbili za eneo la magharibi mwa nchi.
Kalonzo alisema viongozi wa kisiasa hasa wa upinzani wanafaa kupewa uhuru na mazingira salama ya kuuza sera zao za siasa sawa na viongozi wengine serikalini, huku akishinikiza serikali kuhakikisha wahuni hao wanakamatwa na kukabiliwa kisheria.
Kiongozi huyo wa upinzani aliongeza kusema, iwapo serikali haitachukua hatua za haraka basi watalazimika kumfungulia mashtaka Waziri wa usalama wa ndani Kichumba Murkomen na Katibu katika Wazira hiyo Raymond Omollo.

Viongozi wa kisiasa washutumu shambilio la kivamizi dhidi ya Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi
Kauli yake iliungwa mkono na Kinara wa chama cha DAP-Kenya Eugine Wamalwa ambaye alisema wahuni wamekuwa wakishambulia viongozi wa upinzani mara kwa mara jambo linalohatarisha usalama wa viongozi.
Katika kanda ya video iliyonaswa kwenye kamera za siri za CCTV siku ya Jumatano, kundi la vijana lilionekana likiingia kwenye mghahawa mmoja kisha kumshambulia na kumjeruhi seneta huyo.
Wakati huo huo Seneta wa Kakamega Bonny Khaluale aliitaka idara ya upelelezi nchini kuzamia suala la uvamizi dhidi ya viongozi unaotekelezwa na vijana wanaoonekana kukodishwa ili kuwanyamazisha wapinzani.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

