National News
Muturi Atemwa Katika Baraza la Mawaziri
Rais William Ruto amefanya mabadiliko kadhaa katika baraza lake la mawaziri na kuwateua watu wengine kushikilia nyadhfa hizo huku aliyekuwa Waziri wa utumishi wa umma nchini Justin Muturi akitemwa nje.
Katika chapisho rasmi la gazeti la serikali ambalo limetiwa saini na mkuu wa utumishi wa umma nchini Felix Koskei, Rais Ruto kwa kuzingatia kipengele cha 152 ibara ya 2 ya katiba, amemteua Hanna Wendot Cheptumo kushikilia Wizara ya Jinsia, utamaduni na turathi.
Mwengine ni Mbunge wa Mbeere Geoffrey Kiringa Ruku ambaye ameteuliwa kushikilia Wizara ya utumishi wa umma nchini, Wizara ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Justin Muturi ambaye ametemwa nje ya baraza la mawaziri.
Kiongozi wa taifa, ametumia mamlaka yake ya kikatiba kwa kuzingatia kipengele cha 152 ibara ya 5{a}, na kufanya uhamisho wa mawaziri kutoka Wizara moja hadi nyingine ambapo Waziri wa mazigira na misitu nchini Adan Duale amehamishiwa Wizara ya Afya nchini huku Deborah Barasa ambaye alikuwa akishinikilia Wizara hiyo akihamishiwa Wizara ya Mazingira na misitu.
Uteuzi huo mpya wa mawaziri pamoja na uhamisho, umejiri siku moja tu baada ya Rais Ruto kufanya kikao na viongozi kutoka mlima Kenya pamoja na viongozi wengine kutoka maeneo ya Magharibi mwa Kenya sawa na kikao tofauti na Viongozi wa kidini.
National News
Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.
Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.
Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.
Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.
Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.
Editor's Picks
Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi
Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.
Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.
Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.
Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.
Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.
Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.
Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

