Connect with us

National News

Kocha wa Stars Ashukuru Mashabiki

Published

on

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee stars Benni McCarthy amesema kwamba walikutana na mpinzani Bora Gabon katika mechi ya kufuzu kombe la Dunia ugani Nyayo siku ya Jumapili.

Haya yanajiri baada ya stars kupokea kichapo Cha magoli 2-1 dhidi ya The panthers na mwalimu ana amini Gabon tayari wa kikosi Bora kuliko stars na Hilo lilionekana.

“Ni kweli tumekutana na timu Bora ambayo tayari imenjeka kwa muda sisi tumefanya mazoezi siku mbili pekee kinyume na wao.”

Kwa upande wake kocha wa Gabon Thierry myomou amesema kwamba mipango ilifanya Kazi kwani Lengo lao lilikua Moja tu kupata ushindi ama sare ugenini kwa bahati mzuri wakaondoka na ushindi.

“Tulikua na Lengo LA kushinda mechi hii kutokea mwanzo ama kama iwe vigumu tupate sare kwa bahati mzuri tumepata alama zote tatu ni furaha kwetu kwani ulikua ni mechi ngumu mbele ya mashabiki wa nyumbani.

“Hata hivyo McCarthy ameshukuru mashabiki wengi waliokitokeza kuipa msukumo stars akikiri tangu akiwa mchezaji hajaona uwanja ukiwa umefurika hivyo akitaka mailtaifa mengine barani Afrika kuiga Hilo.

“Nichukue fursa kushukuru mashabiki wameonyesha jinsi gani wana upendo kwa timu yetu inasikitisha hatujawapa tabasamu wanaporudi nyumbani ila niwahakikishie nanjenga timu ambayo itaeletea Raha mashabiki wa nyumbani siku za usoni.”

Stars kwa Sasa wanaketi nafasi ya nne kundi F wakiwa na alama sita , Ivory coast wako kileleni na alama 16 baada ya ushindi dhidi ya Gambia nayo Gabon ni ya pili na alama 15 Burundi ni ya tatu na lama 7.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577

Published

on

By

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.

Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.

Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.

Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.

Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.

Continue Reading

Editor's Picks

Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.

Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.

Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.

Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.

Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.

Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.

Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

Continue Reading

Trending