Connect with us

News

Ndoto ya Matiang’i kuwania urais 2027 yaingia doa

Published

on

Mbunge wa Gem Elisha Odhiambo ametangaza mipango ya kumchukulia hatua za kisheria aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang’i kutokana na madai ya mauaji ya kiholela wakati wa utawala wa serikali ya Jubilee.

Mbunge huyo alifichua kuwa anakamilisha ombi la kutaka kumzuia Dkt. Matiang’i kuwania urais, akimwajibisha kwa kile alichokitaja kama dhuluma zilizoidhinishwa na serikali – haswa kutupwa kwa miili katika Mto Yala.

“Kama mbunge wa Gem, nilifanya mkutano na mawakili jana usiku baada ya kusikiliza kauli ya Matiang’i akithibitisha kuwa Wakenya kadhaa waliouawa kwa kuchinjwa walitupwa kwenye mto Yala, tunaenda katika mahakama ya rufaa ili tuweze kumshtaki kama mtu binafsi kwa miile kutupwa kwenye mto Yala ili awajibike kama afisa wa zamani wa afisi ya usalama wa kitaifa,” ilisema Odhiambo.

Odhiambo alimshutumu waziri wa zamani wa mambo ya Ndani kwa kusimamia utawala wa ugaidi uliosababisha uharibifu wa mazingira na kibinadamu katika baadhi ya maeneo ya eneo bunge la Gem.

Alidai kuwa miili mingi iligunduliwa ikiwa imetupwa katika mto Yala wakati wa uongozi wa Matiang’i, akitaja tukio hilo kama “ugaidi wa mazingira” na doa kwa ustawi wa jamii.

Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na runinga moja nchini siku ya Jumanne mwezi juni 2, 2025, Matiang’i alisema alifuatilia suala la miili ya River Yala kwa Inspekta Jenerali wa polisi wakati huo Hillary Mutyambai, ambaye alishikilia kuwa walihitaji familia hizo kutambua miili hiyo ili kufichua ukweli.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending