News
Ndoto ya Matiang’i kuwania urais 2027 yaingia doa
Mbunge wa Gem Elisha Odhiambo ametangaza mipango ya kumchukulia hatua za kisheria aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang’i kutokana na madai ya mauaji ya kiholela wakati wa utawala wa serikali ya Jubilee.
Mbunge huyo alifichua kuwa anakamilisha ombi la kutaka kumzuia Dkt. Matiang’i kuwania urais, akimwajibisha kwa kile alichokitaja kama dhuluma zilizoidhinishwa na serikali – haswa kutupwa kwa miili katika Mto Yala.
“Kama mbunge wa Gem, nilifanya mkutano na mawakili jana usiku baada ya kusikiliza kauli ya Matiang’i akithibitisha kuwa Wakenya kadhaa waliouawa kwa kuchinjwa walitupwa kwenye mto Yala, tunaenda katika mahakama ya rufaa ili tuweze kumshtaki kama mtu binafsi kwa miile kutupwa kwenye mto Yala ili awajibike kama afisa wa zamani wa afisi ya usalama wa kitaifa,” ilisema Odhiambo.
Odhiambo alimshutumu waziri wa zamani wa mambo ya Ndani kwa kusimamia utawala wa ugaidi uliosababisha uharibifu wa mazingira na kibinadamu katika baadhi ya maeneo ya eneo bunge la Gem.
Alidai kuwa miili mingi iligunduliwa ikiwa imetupwa katika mto Yala wakati wa uongozi wa Matiang’i, akitaja tukio hilo kama “ugaidi wa mazingira” na doa kwa ustawi wa jamii.
Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na runinga moja nchini siku ya Jumanne mwezi juni 2, 2025, Matiang’i alisema alifuatilia suala la miili ya River Yala kwa Inspekta Jenerali wa polisi wakati huo Hillary Mutyambai, ambaye alishikilia kuwa walihitaji familia hizo kutambua miili hiyo ili kufichua ukweli.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

