Connect with us

News

Upasuaji wa maiti wagundua vipande 4 vya risasi kichwani.

Published

on

Ripoti ya upasuaji wa maiti ya mchuuzi wa barakoa aliyepigwa risasi kwa karibu na maafisa wa polisi wakati wa maandamano jijini Nairobi imebaini kuwa vipande 4 vya risasi vilibaki kwenye ubongo wa mchuuzi huyo Boniface Kariuki Mwangi.

Upasuaji wa maiti uliofanywa Alhamisi Julai 3, 2025 ulibaini kuwa Kariuki alifariki kutokana na majeraha ya kichwa yaliyosababishwa na risasi aliyopigwa na polisi siku hiyo.

Shughuli ya upasuaji huo iliendeshwa na wapasuaji wakiongozwa na daktari wa serikali Bernard Media kwa kushirikiana na daktari wa familia Peter Ndegwa.

Madaktari hao walibaini kuwa vipande vingine viwili viliondolewa na madaktari wakati Mwangi alipokuwa hai.

Uchunguzi huo haukuweza kuthibitisha kwa uhakika wakati halisi wa kifo chake huku madakrati wakieleza kuwa ubongo wa Mwangi huenda ulikuwa umekufa siku kadhaa kabla ya familia kuarifiwa rasmi.

Maafisa wa polisi wanaohusishwa na tukio hilo wanaendelea kuzuiliwa na polisi.

Mwangi alipigwa risasi na polisi wakati wa maandamano ya kushinikiza naibu inspekta wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu, kufiatia kifo cha mwanablogu na mwalimu Albert Ojwang’.

Baadaye Lagat alijiondoa ofisini kwa mda ili kupisha uchunguzi kuhusiana na mauaji hayo, japo shinikizo za kuondoka ofisini kabisa ziliendelea kupitia maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z.

Mwanablogu huyo Ojwang’ atazikwa Julai 4, 2025 nyumbani kwao kaunti ya Homa bay.

Taarifa ya Joseph Jira.

 

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending