Connect with us

Business

Uhaba wa Samaki Wakumba Sekta ya Uvuvi Malindi

Published

on

Sekta ya uvuvi katika mji wa Malindi kaunti ya Kilifi, inaendelea kukumbwa na changamoto  kufuatia upepo mkali unaovuma baharini kwa kipindi cha wiki kadhaa sasa, hali inayosababisha uhaba mkubwa wa samaki sokoni na kuporomoka kwa mapato ya wavuvi.

Kwa mujibu wa Yunus Aboud Sahe, Mwenyekiti wa ufuo wa bahari katika eneo la Shella, upepo huo ulilazimu wavuvi wengi kusitisha shughuli zao za kila siku kutokana na hatari ya kuzama au kupata ajali baharini.

Sahe alisema kuwa hali hiyo imesababisha idadi kubwa ya wavuvi kukaa nyumbani, jambo ambalo linaathiri vibaya mapato yao na ustawi wa familia zao.

“Kwa sasa, hata wale wachache wanaothubutu kuingia baharini wanarejea na wastani wa kilo mbili pekee za samaki, licha ya kuhatarisha maisha yao. Hii ni hali ngumu kiuchumi na inahitaji suluhisho la haraka,” alisema Sahe.

Aidha, aliwasihi wavuvi hasa wanaovua katika maji ya kina kirefu kuwa waangalifu na kutoingia baharini wakati wa upepo mkali, bali wawe na subira hadi hali ya anga itakapokuwa salama.

Alisisitiza umuhimu wa kuzingatia tahadhari ili kuepuka majanga ambayo yamekuwa yakishuhudiwa mara kwa mara katika eneo hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Biashara ya Mananasi yakabiliwa na changamoto Kilifi

Published

on

By

Wafanyibiashara kuuza matunda aina ya Nanasi kaunti ya Kilifi wanasema biashara ya matunda hayo inazidi kudorora msimu huu ikilinganishwa na msimu uliopita.

Kulingana na wafanyibiashara hao, matunda ya Mananasi hayapatikana kwa urahisi sokoni kutokana na mabadiliko ya hali ya angani licha ya biashara ya matunda hayo kuwa na thamani kubwa katika soko la Pwani na taifa.

Wakiongozwa na Japhet Khambi, wafanyibiashara hao walisema kwa sasa wanategemea matunda hayo kutoka nje ya nchi hasa taifa la Uganda ambapo uagizaji wa matunda hayo umekuwa ghali mno.

Katika suala la usafirishaji wa bidhaa hiyo katika soko la kaunti ya Kilifi kutoka taifa hilo jirani la Afrika Mashariki, wafanyibiashara hao walisema ghamara ya usafiri uko juu mno hali ilichangia bei ya bidhaa hizo kuongezeka mara dufu.

“Hii mambo ya gharama ya usafirishaji na uhaba wa matunda hayo bei ya bidhaa hiyo imepanda kwa kiwango kikubwa, alieleza Khambi.

Wafanyibiashara wa matunda ya Mananasi walisema Nanasi ambalo lilikuwa Linanunuliwa kwa shilingi 100 sasa tunda hilo limepanda bei na kuuzwa kwa shilingi 250.

“ Tulikuwa tunanunua Mananasi kutoka eneo la Chakama katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kwa bei nafuu lakini kwa sasa hayapatikani na kutulazimu kuangiza matunda kutoka Uganda.”, alisema Khambi.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending