Connect with us

Business

Ukaguzi wa maonyesho ya Kilimo Mombasa unaendelea

Published

on

Kamati ya habari na mawasiliano bungeni ikiongozwa na mwenyekiti Wahome Wamatinga imefanya ziara yake katika uwanja wa maonyesho ya kilimo eneo la Nyali kaunti ya Mombasa.

Wamatinga ambaye pia ni Seneta wa Nyeri alisema ziara hiyo inalenga kutathmini maandalizi ya maonyesho ya kilimo ya mwaka huu ambayo yanatarajiwa kuanza tarehe 3 hadi 7 mwezi wa Septemba.

Wamatinga pia alisema wanapania kuweka kibanda maalumu ambacho kitatoa mafunzo ya utendaji kazi wa bunge kwa wale ambao watahudhuria maonyesho hayo.

“Tumekagua mahali ambapo tutakuwa tukijenga kibanda chetu na tumejadiliana yale mambo ambayo tutakuwa tukiyaonyesha’’ alisema Wamatinga.

Naye Mbunge wa Nyali Mohamed Ali alisema kibanda hicho kitatoa huduma zote za bunge kwa Wakenya ambao watahudhuria maonyesho hayo kauli ambayo iliungwa mkono na Mbunge wa Likoni Mishi Mboko ambaye aliwashinikiza wapwani kuhakikisha wanahudhuria maonyesho hayo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Bei za mafuta kuongezeka katikati ya mwezi aprili

Published

on

By

Kenya sasa inakabiliwa na hatari ya kupanda kwa bei za mafuta, huku mgogoro unaoendelea mashariki ya Kati ukianza kuathiri bei nchini.

Serikali sasa imeonya kuwa kufikia katikati ya mwezi Aprili, bei za mafuta huenda zikapanda ikionya kuwa ongezeko la bei ya mafuta kwa sasa haliwezi kuepukika kufuatia kupanda kwa bei za mafuta kimataifa.

Waziri wa hazina kuu ya kitaifa John Mbadi aliwahakikishia wakenya kuwa hakuna cha kuhofia kwani wameweka mikakati kupunguza athari zake.

Ili kupunguza athari za bei za mafuta kuongezeka, serikali ilisema itatumia shilingi bilioni 17 kutoka mfuko wa ada ya uwekezaji wa mafuta kusaidia kudhibiti bei kwa mda wa miezi 3 ijayo.

Kwa sasa serikali inasema kuna akiba ya kutosha ya mafuta na shehena zaidi zinatarajiwa nchini hivi karibuni.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Business

KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa

Published

on

By

Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.

Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.

Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending