News
Kikao cha wabunge wa UDA na ODM chafanyika Nairobi
Rais William Samoei Ruto pamoja na Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga wameongoza kikao cha pamoja cha wabunge wa chama ODM na UDA katika eneo la Karen Jijini Nairobi.
Akizungumza katika kikao hicho, Rais Ruto aliwahimiza wabunge wa vyama hivyo viwili kushirikiana ili taifa la Kenya liweze kusonga mbele kimaendeleo na akawataka viongozi kuweka maslahi ya Wakenya mbele kuliko siasa za vyama na ubinafsi.
Rais Ruto alisema ni kupitia umoja ndipo ajenda za serikali zitafanikishwa ipasavyo na kuwapongeza wabunge na Maseneta kwa kupitisha miswada mbalimbali kama wa afya ambao umekuwa wenye manufaa kwa Wakenya.
“Hili sio suala la Williama Ruto. Leo niko kesho sitakuwa. Sio pia kuhusu Raila Odinga bali ni kwa ajili ya nchi inayoitwa Kenya ambapo tuko na fursa nzuri ya kufanya maamuzi yanayofaa kwa ajili ya nchi hii’’ alisema Rais Ruto
Ni kauli ambayo iliungwa mkono na Raila Odinga ambaye aliwataka wabunge wa vyama hivyo kuweka kando tofauti zao za kisiasa ili kuafikia hayo.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

