Connect with us

News

Vijana waahidi kupigania mageuzi wanapojisajili kama wapiga kura wapya

Published

on

Zoezi endelevu la kusajili wapiga kura wapya limeanza rasmi kote nchini huku idadi kubwa ya vijana wakijitokeza katika zoezi katika maeneo mbalimbali nchini.

Mjini Kilifi katika kaunti ya kilifi, vijana walijitokeza katika kituo cha usajili tawi la eneo bunge la Kilifi kaskazini, wengi wakisema wanataka kupigania mageuzi katika uongozi wa nchi hasa wakati wa uchaguzi mkuu ujao wa 2027.

Vijana hao wamliambia Coco Fm kwamba wanataka kuleta mwamko mpya wa uongozi kwa kubadili viongozi ambao wameonekana kutojali maslahi ya mwananchi mpiga kura.

Walidai viongozi wengi walioko madarakani kwa sasa wameshindwa kutekeleza ahadi walizotoa kwa mpiga kura, wakishinikiza vijana wenzao kujitokeza kwa wingi kusajiliwa katika zoezi hilo.

“Matarajio yangu nikuwa tutapata viongozi bora, Kilifi tunahitaji viongozi wenye wataleta maendeleo pia ndio maana pia nimefanya maamuzi ya kuja kukata kadi ya kura”, alisema Purity Apiya mkaazi wa kilifi.

Baadhi ya vijana waliojitokeza kwenye zoezi la usajili wa wapiga kura mjini Kilifi.

Kwa upande wake Abdhul Mohammed Issa, Naibu msajili katika tume ya IEBC eneo bunge la Kilifi Kaskazini aliesema wanasajili watu ambao hawajasajiliwa kabisa pamoja na wale wanaotaka kubadili vituo vya kupigia kura.

“Tutakuwa tunaandikisha watu upya wale ambao hawajakata kabisa, wale ambao wanataka kubadilisha vituo vya vya kupigia kura, tuseme mtu anataka kuhama kituo chake tunamhamisha ama kama ni mtu anataka kuhama eneo lake la bunge pia tunamhamisha”, alisema Issa

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending