News
Vijana waahidi kupigania mageuzi wanapojisajili kama wapiga kura wapya
Zoezi endelevu la kusajili wapiga kura wapya limeanza rasmi kote nchini huku idadi kubwa ya vijana wakijitokeza katika zoezi katika maeneo mbalimbali nchini.
Mjini Kilifi katika kaunti ya kilifi, vijana walijitokeza katika kituo cha usajili tawi la eneo bunge la Kilifi kaskazini, wengi wakisema wanataka kupigania mageuzi katika uongozi wa nchi hasa wakati wa uchaguzi mkuu ujao wa 2027.
Vijana hao wamliambia Coco Fm kwamba wanataka kuleta mwamko mpya wa uongozi kwa kubadili viongozi ambao wameonekana kutojali maslahi ya mwananchi mpiga kura.
Walidai viongozi wengi walioko madarakani kwa sasa wameshindwa kutekeleza ahadi walizotoa kwa mpiga kura, wakishinikiza vijana wenzao kujitokeza kwa wingi kusajiliwa katika zoezi hilo.
“Matarajio yangu nikuwa tutapata viongozi bora, Kilifi tunahitaji viongozi wenye wataleta maendeleo pia ndio maana pia nimefanya maamuzi ya kuja kukata kadi ya kura”, alisema Purity Apiya mkaazi wa kilifi.

Baadhi ya vijana waliojitokeza kwenye zoezi la usajili wa wapiga kura mjini Kilifi.
Kwa upande wake Abdhul Mohammed Issa, Naibu msajili katika tume ya IEBC eneo bunge la Kilifi Kaskazini aliesema wanasajili watu ambao hawajasajiliwa kabisa pamoja na wale wanaotaka kubadili vituo vya kupigia kura.
“Tutakuwa tunaandikisha watu upya wale ambao hawajakata kabisa, wale ambao wanataka kubadilisha vituo vya vya kupigia kura, tuseme mtu anataka kuhama kituo chake tunamhamisha ama kama ni mtu anataka kuhama eneo lake la bunge pia tunamhamisha”, alisema Issa
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

