Connect with us

News

Justine Muturi aibua wasiwasi kuhusu sajili ya wapiga kura

Published

on

Kinara wa Chama cha Democratic Party (DP) Justine Muturi ameibua wasiwasi kuhusu uwezekano wa kuhitilafiana na sajili ya wapiga kura kufuatia makubaliano kati ya tume huru ya uchaguzi na mipakani nchini IEBC na data ya sajili ya kitaifa ya watu NRB.

Muturi, alihoji kwamba makubaliano kati ya tume ya IEBC na NRB ambayo iko chini ya ofisi ya rais kuhusu kushirikiana na taarifa za data ni njama ya uwezi wa kura, akisema ataweka wazi suala hilo kwa umma.

Muturi alisema kuna taarifa kwamba afisa mkuu mtendaji wa tume ya IEBC Moses Sankuli amekuwa akifanya mikutano ya siri na maafisa wa sajili ya kitaifa ya watu NRB ili kubaini data kamili na pia amekuwa kishirikiana na kampuni binafsi za kieletroniki kama vile Smartmatic.

Kiongozi huyo alisema makubaliano yeyote yasio na uwazi yanayohusisha ofisi ya rais, hasa katika masuala yanayohusu taarifa za usajili wa wapiga kura na hifadhi data, yanatishia uadilifu, kuaminika na uwazi wa mchakato wa uchaguzi.

Akijibu tuhuma hizo, mwenyekiti wa tume ya IEBC Erastus Ethekon alisema mipango ya kushirikisha data na taasisi za umma za kibinafsi hufanyika chini ya mifumo madhubuti ya kisheria ili kuzuia udanganyifu, huku washirika wakipewa taarifa mara tu mchakato huo unapokamilika.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mpango wa uagizaji mafuta wa G to G waingia dosari

Published

on

By

Serikali imeendelea kujitetea kuhusu mpango wa uagizaji wa mafuta wa serikali kwa serikali maarufu kama G to G, huku viongozi wa kisiasa wakitoa mitazamo kinzani kuhusu utekelezaji wake.

Serikali kupitia Mamlaka ya kudhibiti bei za mafuta nchini EPPRA, imetangaza ongezeko la bei mpya za mafuta kwa shilingi 28 kwa lita moja ya mafuta ya petrol huku diseli ikiongezeka kwa shilingi 40 kwa lita.

Hatua hii imezua mjadala mkali kuhusu athari za mfumuko wa bei nchini.

Viongozi wa upinzani wakiongozwa na Kinara wa Chama cha DCP, Rigathi Gachagua, na Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka wamekosoa vikali serikali kufutia ongezeko la bei ya mafuta wakisema mpango wa G to G ilikuwa ni njama ya kumfaidi Rais William Ruto, wakifichua kwamba takriban shilingi tano kwa kila lita ya mafuta itakayouzwa nchini itakuwa inamfaidi Rais Ruto.

Viongozi hao pia, walimtaka Waziri wa Kawi na Petroli nchini Opiyo Wandayi, pamoja na Waziri wa Biashara na Uwekezaji wa viwanda nchini Lee Kinyanjui, kujiuzulu.

Kwa upande wake mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro pia ameukosoa mpango huo akidai kwamba ni njama ya baadhi ya viongozi wakuu serikalini kujinufaisha binafsi.

Nyoro aliema mpango huo ni njia ya kuwahadaa wakenya ilhali mzigo mkubwa unaishia kwa walipa ushuru.

Aliongeza kuwa mpango huo unanufaisha baadhi ya kampuni za mafuta nchini zinazodaiwa kumilikiwa na viongozi wa juu serikalini huku akitoa baadhi ya mapendekezo kwa serikali pamoja na wadau wa sekta ya kawi ambayo kulingana naye, yanaweza kushusha bei ya mafuta kwa takriban shilingi 27.

Hata hivyo, Rais William Ruto ametetea mpango huo akisema serikali imetumia takriban shilingi bilioni 6.5 kutoa ruzuku ya mafuta ili kupunguza mzigo kwa wananchi hasa ushuru wa VAT kwa asilimia 8.

Kwa upande wake, Waziri wa Kawi na Petroli nchini Opiyo Wandayi alisema serikali imejizatiti kukabiliana na wanaojihusisha na uagizaji wa mafuta ghushi humu nchini.

Hata hivyo, kumeshuhudiwa tofauti katika takwimu za fedha zilizotolewa kuhusu mpango huo, Rais akitaja bilioni 6.5 ilhali Waziri Wandayi akisema serikali iliwekeza takriban bilioni 6.2.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

News

IEBC: Vijana wanaitisha pesa kusajiliwa kuwa wapiga kura

Published

on

By

Wakenya wanaojitokeza kujisajili kama wapiga kura katika zoezi endelevu lililoidhinishwa na Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, inatia matumaini ya Tume hiyo kufikia malengo yake ya kusajili wa idadi ya watu milioni 6.2 kote nchini.

Katika kaunti ya Kilifi kwenye eneo bunge la Kilifi Kazkazini ambapo zoezi hilo linaendelea, Maafisa wa Tume hiyo wamedai kupitia changamoto wakati wa usajali wa wapiga kura.

Maafisa hao wanasema kati ya changamoto hizo ni pamoja na kuitishwa pesa na vijana ndipo wawasajili kuwa wapiga kura, wakisema changamoto hiyo inarudisha nyuma juhudi zilizoidhinisha na Tume ya IEBC.

Afisa anayesimamia Tume ya IEBC katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini John Mwawasi alisema licha ya changamoto hizo, kufikia sasa maafisa wa tume hiyo wanaozuru nyanjani wamefanikiwa kusajili wapiga kura wapya kwa asilimia 50.

Mwawasi alisema japo wanalenga kusajili idadi ya wakenya zaidi ya elfu 13 katika eneo bunge hilo, kufikia sasa wamesajili wakenya zaidi ya elfu 6.
“Changamoto ambayo tunapitia kwa sasa ni vijana ambao tunalenga kuwasajili wamekuwa wakiitisha pesa maafisa wetu ili wasajiliwe kuwa wapiga kura wapya lakini tumekuwa tukiwaeleza kwamba zoezi hili ni hiari na kwamba litawapa nafasi nzuri ya kufanya mabadiliko ya kiuongozi kuanzia ngazi ya kitaifa hadi mashinani”,alisema Mwawasi.
Wakaazi waliokuwa wamefika katika ofisi za IEBC kusajiliwa wameelezea wepesi wa zoezi hilo, kutokana na maafisa hao wanatumia mfumo wa kieletronic.
Tume hiyo ya IEBC imejitenga na masuala ya kujihusisha na siasa na kuwarai wanasiasa kuwasaidia katika kuwarai wananchi hasa vijana kujisajili kama wapiga kura, kauli ambayo imeungwa mkono na Naibu Mwenyekiti wa IEBC Fahima Araphat.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
Continue Reading

Trending