Connect with us

News

Justine Muturi aibua wasiwasi kuhusu sajili ya wapiga kura

Published

on

Kinara wa Chama cha Democratic Party (DP) Justine Muturi ameibua wasiwasi kuhusu uwezekano wa kuhitilafiana na sajili ya wapiga kura kufuatia makubaliano kati ya tume huru ya uchaguzi na mipakani nchini IEBC na data ya sajili ya kitaifa ya watu NRB.

Muturi, alihoji kwamba makubaliano kati ya tume ya IEBC na NRB ambayo iko chini ya ofisi ya rais kuhusu kushirikiana na taarifa za data ni njama ya uwezi wa kura, akisema ataweka wazi suala hilo kwa umma.

Muturi alisema kuna taarifa kwamba afisa mkuu mtendaji wa tume ya IEBC Moses Sankuli amekuwa akifanya mikutano ya siri na maafisa wa sajili ya kitaifa ya watu NRB ili kubaini data kamili na pia amekuwa kishirikiana na kampuni binafsi za kieletroniki kama vile Smartmatic.

Kiongozi huyo alisema makubaliano yeyote yasio na uwazi yanayohusisha ofisi ya rais, hasa katika masuala yanayohusu taarifa za usajili wa wapiga kura na hifadhi data, yanatishia uadilifu, kuaminika na uwazi wa mchakato wa uchaguzi.

Akijibu tuhuma hizo, mwenyekiti wa tume ya IEBC Erastus Ethekon alisema mipango ya kushirikisha data na taasisi za umma za kibinafsi hufanyika chini ya mifumo madhubuti ya kisheria ili kuzuia udanganyifu, huku washirika wakipewa taarifa mara tu mchakato huo unapokamilika.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending