News
Gachagua amshtuma IG Kanga kuhusu usalama wa Ol Kalou
Kinara wa Chama cha Democracy for Citizens Party (DCP), Rigathi Gachagua, amemshutumu Inspekta Jenerali wa Polisi, Douglas Kanja, kwa kusimamia operesheni ya usalama inayodaiwa kulenga kuvuruga uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Ol Kalou utakaofanyika siku ya Alhamisi, Julai 16, 2026
Gachagua alidai kwamba kupelekwa kwa zaidi ya maafisa wa polisi 1,000 kunalenga kushawishi matokeo ya uchaguzi huo kuegemea upade mmoja wa mrengo wa kisiasa.
Katika barua aliyomuandikia Inspekta Jenerali siku ya Jumatano Julai 15, 2026, Gachagua alidai kwamba uongozi wa huduma ya kitaifa ya Polisi umeingiliwa na kuathiriwa, na kwamba operesheni za usalama zinaelekezwa na maafisa wakuu serikalini badala ya uongozi wa maafisa wa Polisi.
Aidha alitilia shaka idadi ya maafisa wa polisi wanalitumwa eneo hilo, akisema ni sawa na kuhujumu haki za wakaazi wa Ol Kalou huku akisisitiza kwamba eneo bunge hilo limekuwa la amani kwa miaka mingi.
Kiongozi huyo alisema matukio yalioshuhudiwa katika eneo bunge hilo wakati wa kipindi cha kampeni za uchuguzi huo, yalilenga wafuasi wa Chama cha DCP.
“Inspekta Jenerali Kanja, inaonekana bado hujaelewa; uongozi wa Huduma ya kitaifa ya Polisi umechukuliwa kabisa na Kipchumba Murkomen, Raymond Omollo na wanasiasa waasi wanaomuunga mkono William Ruto,” alisema.
Gachagua ambaye alikuwa kuwa Naibu rais, alisema tabia ya maafisa wa polisi kukosa kuwachukulia hatua wahuni ni sawa na kuruhusu taifa kuingia katika utawala wa wahuni jinsi ilivyoshuhudiwa nchini Haiti.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Waliodai kupotezewa nyeti wahukumiwa mwaka mmoja gerezani
Mahakama ya Kilifi imewahukumu kifungo cha mwaka mmoja gerezani baba na mwanawe wanaohusishwa na kesi ya tuhma za kupotea kwa sehemu nyeti.
Wawili hao Benson Ngala Daniel na Ruphus Chai walishtakiwa na kesi ya kumpiga na kumjeruhi vibaya mama mmoja kwa jina Asha Samini waliyedai kuwa alikuwa amewaibia sehemu nyeti baada ya kuwasalimia
Hukumu hiyo imetolewa baada ya upande wa mashtaka ukiongozwa na Nancy Njeru kuiomba Mahakama itilie maanani kesi hiyo, akisema kuwa uvumi unaoendelea Kilifi na Pwani kwa jumla kwamba watu kupotezewa nyeti umesababisha vifo na wengine kuachwa na majeraha mabaya huku wakiibiwa mali zao.
Akitoa hukumu hiyo, Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike amesema kuwa kifungo hicho kitakuwa funzo kwa watu wote wanaopiga watu kwa kuwatuhmu uchawi wa kuiba sehemu nyeti.
Awali upande wa mashtaka ulielezea mahakama kwamba mnamo tarehe 5 mwezi huu wa Julai, eneo la Mdangarani eneo la Kauma kaunti ya Kilifi, Benson na Ruphus walimpiga vibaya mlalamishi hali iliyomsababishia majeraha mabaya na ya kudumu na sasa anaendelea na matibabu katika hospitali ya rufaa Kilifi.
Aidha Mahakama imeagiza mlalamishi kuendelea na matibabu na kupata ushauri nasaha kupitia ofisi ya jamii.
Wahukumiwa wamepewa siku 14 za kukata rufaa.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
IEBC: Uchaguzi wa Ol Kalou utakuwa huru na haki
Baada ya kushuhudiwa kampeni za vurugu, hongo na uchochezi dhidi ya wananchi wa eneo bunge la Ol Kalou kaunti ya Nyandurua kabla ya uchaguzi mdogo, sasa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC inasema imejipanga vyema kuandaa uchaguzi huo mdogo wa eneo bunge hilo.
Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon, alijitokeza kwa kishindo na kuanza kwa kutoa onyo kali kwa wagombea wote wanaomezea mate kiti hicho.
Katika kikao na Wanabahari, Ethekon alisema IEBC inachukulia kwa uzito sajili ya wapiga kura, na akawaonya wananshi dhidi ya kuwachochea wananchi kufisha vitambulisho vyao, akisema tabia hiyo haitakubalika.
“Tunachukulia kwa uzito sana sajali ya wapiga kura ya Ol Kalou na tunatoa onyo kali kwa wagombea wote wanaomezea mate kiti hicho kuzingatia sheria na kwmaba tutaruhusu ajenti mmoja pekee katika kituo cha kupigia kura na hakuna mtu anaruhusiwa kupiga picha”, alisema Ethekon.
Kwa upande wake Inspekta Jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja aliwaonya vijana dhidi ya kushawishiwa vibaya na kuvuruga zoezi la uchaguzi huo mdogo, akisema tayari zaidi ya maafisa wa polisi elfu moja wametumwa Ol Kalou kushika doria.
“Tuko na maafisa wa zaidi ya elfu moja tumewatuma Ol Kalou kushika doria na tunawaonya vijana dhidi ya kushawishi vibaya na kuvurugu zoezi la uchaguzi huo, hiyo hatutakubali. Tunataka uchaguzi uwe wa amani”, alisema Kanja.
Mwenyekiti wa Tume ya uwiano na utangamano wa kitaifa NCIC Kepha Omae amewataka wanasiasa kukoma kuwachochea wananchi na kukumbatia amani, akisema Kenya inahitaji utulivu kuliko siasa za chuki.
Uchaguzi huo mdogo wa eneo bunge la Ol Kalou umeratibiwa kufanyika Julia 16 siku ya Alhamis huku zaidi ya wapiga kura elfu 72 wakiwa wamesajli, IEBC ikisema vifaa vya kupigia kura vitasambazwa siku ya Jumatano chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

