Sports
Kocha Nyamunyamu Tulikosa Taji Kwani Wachezaji Waliondoka
Kocha wa kilabu ya akina dada Vihiga Queens ya Magharibi Bonface Nyamunyamu amesema kwamba kwa sasa wanaangazia kupata taji la akina dada FKF Cup baada ya ligi ya akina dada KWPL kuwaponyoka msimu huu.
Akizungumza na Kipenga cha COCO FM mwalimu huyo amekiri ilikua vigumu wao kumaliza kileleni kutokana na mabadiliko makubwa kikosini msimu uliopita.
“Ligi ilikua ngumu kwetu kushinda msimu huu kwa sababu tulipoteza wachezaji wengi mahiri ,tulipoteza kipa wetu namba moja ,tukapoteza pia mabeki wetu tegemeo wawili kwa wapinzani wetu pia tukapoteza mshambulizi wetu mahiri haya yote ukiweka kwa pamoja yalitatiza kikosi changu kwani ilibidi tuanze upya na wachezaji wengine.”
Hata hivyo mwalimu huyo sasa anaamini na kikosi walichonacho watakuwa vizuri msimu ujao kupigania ubingwa wa ligi ambayo imewaponyoka tangu mwaka 2021.
Kilabu hiyo ilimaliza nafasi ya 4 msimu uliokamilika na alama 38 ligi iliotwaliwa na kilabu Kenya Police Bullets.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

