News
Kenya yaadhimisha sherehe za 63 za Madaraka
Rais William Samoei Ruto amewaongaza wakenya kuadhimisha sherehe za kitaifa za 63 za Madaraka katika kaunti ya Wajir.
Hatua hii ni ya kihistoria kuwa kufanyika katika kaunti ya Wajir tangu taifa lijipatie uhuru kinyume na maeneo mengine ya taifa hili la Kenya.
Kaunti ya Wajir ni kati ya kaunti zinazopatika katika maeneo ya Kaskazini mwa Kenya na maeneo ambayo mara nyingi yamekuwa yakishuhudia misururu ya mashambulizi ya kigaidi, lakini kutoka na serikali kuchukua hatua ya kuimarisha usalama katika maeneo hayo, sasa wakaazi wa kaunti hizo wamaanza kushuhudia matunda miradi ya maendeleo.
Wakati wa halfa hiyo iliyohudhuria na wakenya zaidi ya elfu 10 katika wanja wa Wajir Stadium, rais William Ruto ambaye ni amri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini, amesema atahakikisha sherehe za kitaifa zinafanyika katika kaunti mbalimbali nchini kinyume na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Katika hotuba yake kwenye sherehe hizo za Madaraka, Rais Ruto amesema tangu taifa la Kenya kupata uhuru eneo hilo lilitelekezwa katika masuala mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Rais William Ruto awaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka kaunti ya Wajir
Rais Ruto pia alisema eneo hilo lilitengwa kwa miaka mingi kwa madai ni eneo kame na hakuna usalama wa kutosha.
“Katika uongozi wangu, nitahakikisha wananchi wa maeneo haya wanapata maendeleo sawa na wengine nchini, na niko na uchunguzi sana kuona watu wa Wajir wametengwa kwa miaka mingi na suala hili halitashuhudiwa tena na usalama utaimarishwa kwa wananchi wote”, alisema Rais
Wakati huo huo, Rais Ruto alisema kila jamii ina haki ya kunufaika na maendeleo nchini bila kubaguliwa na kuomba msamaha wenyeji wa kaunti ya Wajir kwa kutelekezwa kwa miaka mingi.
News
Baraza la Jamii ya Sekuye lalamikia uchimbaji wa madini kiholela
Baraza la Wazee wa jamii ya Sekuye eneo la Moyale kaunti ya Marsabit limejitokeza na kulalamikia kuharibiwa kwa mazingira ya maeneo yao hasa katika kijiji cha Dabel kutokana na uchimbaji madini kiholela.
Wazee hao wamewalaumu viongozi wao ikiwemo serikali ya kaunti kwa kulinyamazia suala hilo huku wakaazi wakiendelea kunyanyaswa raslimali zao.
Baraza hilo, chini ya Katibu wake mkuu Haji Hassan Tepo, limedai kwamba uchimbaji huo wa madini kiholela, unyakuzi wa ardhi, unyanyasaji wa jamii umechangiwa na baadhi ya wawekezaji kutoka taifa Jirani la Somalia na Ethiopia ambao hawana vibali halali.
Hassan aliimtaka serikali kupitia Waziri wa madini nchini Hassan Ali Joho kuingilia kati suala hilo na kuhakikisha uchumbaji wa madini katika kijiji cha Dabel unasitishwa kwani wawekezaji zaidi ya 20 wamebuni makundi na kuendelea kuwanyanyasa wenyeji.
Hassan aliweka wazi kwamba baraza hilo pamoja na jamii ya Sekuye linapinga mpango huo na kusisitisha kwamba hawatakubali ardhi yao wanayoitegemea kwa shughuli mbalimbali kutumika vibaya.
Naibu Mwenyekiti wa baraza hilo Abdukadir Dilo alisema hali hiyo imewasabibishia hasara kwani mifugo imeangamia, uchumi wa kijiji hicho ukididimia zaidi na akamtaka rais Ruto kuingilia kati kwani licha ya Waziri Murkomen kufunga uchumbaji kufuatia utovu wa usalama bado wawekezaji kutoka Ethiopia na Somali wamekuwa wakiendeleza mpango huo.
Wazee hao hata hivyo walisisitiza kwamba hawatakubali kuachilia ardhi yao kunyakuliwa na watu wanaodai kuwa wawekezaji ilhali vijana wa eneo hilo hawana kazi, huku wanafunzi wakiacha shule na zaidi ya akina mama 22 wakiachwa na wanaume zao kufuatia suala hilo katika kijiji cha Dabel.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Murkomen ahimiza ushirikiano wa pamoja na wadau wa masuala ya ubaharia
Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya washirika na wadau ili kuimarisha usalama wa baharini na maziwa makuu.
Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la kamati ya uongozi wa Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS) lililofanyika mjini Mombasa, Waziri huyo alisisitiza kuwa ushirikiano wa mapema ni muhimu katika kukabiliana na vitisho vinavyoibuka vya usalama wa baharini.
“Ushirikiano wa mapema na muhimu katika kulinda usalama wetu wa baharini,” alisema Murkomen.
Kongamano hilo la siku tatu linaandaliwa kwa pamoja na huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya (KCGS) pamoja na mradi wa njia muhimu za baharini wa Indo-Pasifiki unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU-CRIMARIO), ukiwaleta pamoja wadau wa usalama wa baharini..
Mradi wa EU-CRIMARIO umeundwa kuimarisha usalama na ulinzi wa baharini kupitia kuboreshwa kwa ushirikiano wa taarifa na uratibu wa operesheni.

Kongamano la siku tatu la kamati ya uongozi la Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS), Mombasa
Mpango wake mkuu, IORIS, ni jukwaa salama na lisiloegemea upande wowote linalotumia mtandao, unaounganisha zaidi ya mashirika 150 kutoka nchi 70, na kuwezesha uratibu wa operesheni za baharini kwa wakati halisi.
Kauli za Murkomen ilijiri kufuatia tangazo la Rais William Ruto kwamba kampuni ya usafiri wa baharini ya Norway, Wilhelmsen, itaajiri mabaharia 1,000 kutoka Kenya, baada ya mazungumzo na kampuni hiyo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkurugenzi wa EU-CRIMARIO Martin Cauchi Inglott, Mkurugenzi mkuu wa huduma ya walinzi wa Pwani ya Kenya Bruno Shioso, Naibu mkuu wa ujumbe wa umoja wa Ulaya nchini Kenya Ondrej Simek, pamoja na washkadau wengine.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

