Connect with us

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Arsenal Ikishinda Kombe Nitampa Main Man Rio Gari na Dadangu – Shuga Boy

Published

on

Mjadala mkali umeibuka katika kipindi cha COCO Asubuhi baada ya Shuga Boy, shabiki wa Manchester United, kuweka dau zito na la kushangaza dhidi ya Main Man Rio ambaye ni shabiki wa Arsenal.

Akizungumza kwenye kipindi cha COCO Asubuhi, kinachoendeshwa na Tatu Sure—inayojumuisha Shuga Boy mwenyewe, Main Man Rio na Solomon Zully—Shuga Boy alifunguka, akidai kuwa Arsenal hawana uwezo wa kubeba hata kombe moja msimu huu licha ya matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki wao.

Kwa mujibu wa Shuga Boy, mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakijipa matumaini makubwa ya kutwaa hadi vikombe vinne, lakini hali halisi uwanjani haioneshi dalili hizo. Alienda mbali zaidi na kuweka dau la kipekee kwa Main Man Rio, ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal.

“Nilimwambia Main Man Rio, wakibeba kombe nitampa gari yangu. Sasa naongeza dau—wakishinda kikombe msimu huu, nitampa gari yangu pamoja na dadangu,” alisema Shuga Boy kwa msisitizo, kauli iliyozua kicheko na mjadala mkali studio.

Kauli hiyo imekuja katika kipindi ambacho Arsenal wamekuwa wakionyesha ushindani mkubwa chini ya kocha Mikel Arteta, wakijijenga kama moja ya timu zinazowania ubingwa wa Premier League. Licha ya maendeleo hayo, ukosefu wa vikombe katika misimu mingi bado unawapa wapinzani wao nafasi ya kuwabeza.

Kwa upande mwingine, Manchester United nao wanapitia kipindi cha mabadiliko, wakijaribu kurejea kwenye ubora wao wa zamani waliouonyesha enzi za Sir Alex Ferguson. Licha ya changamoto, bado wana historia nzito ya mafanikio, jambo linalowapa mashabiki wao kujiamini wanapojadili soka la Uingereza.

Usiku wa leo, macho ya mashabiki yataelekezwa kwenye mchezo wa ligi kati ya Manchester United dhidi ya Leeds United—mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku Shuga Boy akitumaini timu yake itapata ushindi na kuendeleza presha kwa wapinzani wao.

Wakati mabishano yakiendelea mitandaoni na kwenye studio za redio, swali kubwa linabaki: Je, Arsenal wataweza kuwanyamazisha wakosoaji wao kwa kubeba angalau kombe moja msimu huu, au kauli ya Shuga Boy itageuka kuwa unabii?

Continue Reading

Entertainment

Watoe Nyingi… Mimi Natoa Moja! Kauli ya King Kiba Yazua Mjadala

Published

on

Staa wa Bongo Fleva Alikiba ameibua mjadala mzito kufuatia kauli yake aliyoitoa baada ya kufanya show kubwa na yenye mafanikio jijini Mwanza, nchini Tanzania.

Baada ya kupanda jukwaani na kuonesha kiwango chake cha juu cha uimbaji na burudani, King Kiba aliacha mashabiki wakizungumza zaidi si tu kuhusu show yake, bali pia kauli yake iliyokuja mwishoni mwa performance yake. Akiwa mbele ya umati mkubwa wa mashabiki, alisema kwa kujiamini:

“Watatoa ngoma nyingine na nyingine, na nyingine, na nyingine, na nyingine… halafu mimi natoa nyingine, moja tu.”

Kauli hiyo imezua tafsiri mbalimbali miongoni mwa mashabiki na wadau wa muziki, wengi wakiona kuwa ni ujumbe unaolenga tofauti iliyopo kati ya wasanii wanaotoa kazi nyingi kwa wakati mfupi na wale wanaochagua kutoa kazi chache lakini zenye ubora wa hali ya juu. Kwa muktadha huo, Alikiba anaonekana kusimama katika kundi la wasanii wanaoamini katika ubora kuliko wingi.

Kwa muda mrefu sasa, Kiba amekuwa akijulikana kwa mtindo wake wa utoaji wa muziki usio wa haraka, lakini unaolenga ubora wa juu na maisha marefu ya kazi zake sokoni. Hii ni tofauti na mwenendo wa sasa wa tasnia ya muziki wa kidigitali ambapo baadhi ya wasanii huchagua kutoa nyimbo mfululizo ili kubaki juu ya chati na kwenye algorithms za streaming platforms.

Kauli yake pia imekuja katika kipindi ambacho wimbo wake mpya Finale, aliomshirikisha Bien, unaendelea kufanya vizuri kwenye majukwaa ya kidigitali. Video ya wimbo huo imekuwa ikipata watazamaji wengi na maoni chanya kutoka kwa mashabiki wa Afrika Mashariki na kwingineko, hali inayoongeza uzito wa ujumbe wake kuwa kazi moja bora inaweza kuwa na athari kubwa kuliko nyingi zisizo na nguvu sawa.

Baadhi ya wachanganuzi wanasema kijembe hicho kimemlenga mpinzani wake wa karibu Diamond Platnumz ambaye ameachia nyimbo mbili (Happy na Joy) kwenye kipindi kifupi ambacho King Kiba kaachia wimbo mmoja unaofanya vizuri zaidi ya nyimbo za Simba.

Hata hivyo, mjadala unaoibuliwa na kauli hiyo una pande mbili. Wapo wanaounga mkono msimamo wa Kiba wakisema ubora ndiyo unaojenga legacy ya msanii. Lakini pia wapo wanaoamini kuwa katika ushindani wa sasa, consistency ya kutoa nyimbo mara kwa mara ni muhimu ili kubaki relevant kwenye soko lenye ushindani mkubwa.

Kwa mtazamo wa kina, kauli ya Alikiba si tu maneno ya jukwaani bali ni tafakari ya mkakati wake wa muziki na namna anavyoiona tasnia kwa ujumla. Inaibua swali muhimu kwa wasanii na mashabiki pia—je, thamani ya msanii ipo kwenye wingi wa kazi anazotoa, au kwenye ubora na uimara wa kazi chache anazoachia?

Hadi sasa, jambo moja liko wazi—kauli hiyo imefanikiwa kuamsha mjadala mkubwa, na kwa mtindo wa King Kiba, huenda hata hilo lenyewe ni sehemu ya mchezo wake wa kisanii.

Continue Reading

Trending