Sports
Martin Zubimendi Kutua Arsenal
Kilabu ya Arsenal imekubaliana na kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 51.
Raia huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 26 sasa anatarajiwa kuwasili mjini London kwa vipimo vya kimatibabu baada ya kukubali kutua Emirates.
Haya yanajiri baada kuwepo kwa ripoti nchini Uhispania kwamba Real Madrid walikua wameingia kwenye kinyanganyiro cha kusaka huduma za kiungo huyo mbunifu.
Kulingana na mkali wa taarifa za Uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano ni kwamba mchezaji huyo amekubali kuwasili London baada kukuabaliana na matakwa yake binafsi na yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano.
Mchezaji huyo atakua sajili wa kwanza msimu huu kwa kocha mkuu Mikel Arteta.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

