Connect with us

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

International News

Rais wa Cameroon amteua mwanawe kuwa makamu wa rais

Published

on

By

Taifa la Cameroon limeidhinisha mabadiliko ya kisheria kuhusu wadhfa wa makamu wa rais na kumpa mamlaka zaidi rais wa taifa hilo kufanya uteuzi upya.

Sheria hiyo mpya, inampa uwezi makamu wa rais kuchukua nafasi ya rais moja kwa moja iwapo rais wa taifa hilo amefariki ama amekubwa na ugonjwa na kushindwa kuendelelea na majukumu yake kama rais kabla ya uchaguzi kuandaliwa.

Bunge la taifa hilo siku ya Jumamosi liliidhinisha mabadiliko hayo ya kisheria na kutoa nafasi ya kuteuliwa kwa makamu wa rais ili kuhakikisha shughuli za kiserikali zinaendeshwa vyema baada ya bunge la kitaifa na seneti kupiga kura na kufanya mabadiliko hayo ya kisheria katika taifa hilo la Cameroon.

Wabunge wa bunge la kitaifa na Seneti nchini Cameroon walipiga kura 200 huku wengine 18 wakipinga na wengine 4 wakikwepa kikao hicho cha bunge, hatua iliyopelekea mswada huo kupitishwa.

Hatua hiyo sasa imefanya Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 kumteua mwanawe Franck Emmanuel Biya kuwa makamu wa kwanza wa rais katika taifa hilo.

Rais wa Cameroon Paul Biya mwenye umri wa miaka 93 na mwanawe Franck Emmanuel aliyemteua kuwa makamu wa rais wa taifa hilo.

Ni hatua ambayo imeibua mjadala mkali nchini Cameroon na bara Afrika kwa jumla baada ya uteuzi huo kutangazwa rasmi Aprili 4, 2026.

Sheria hiyo pia imepiga marufuku wananchi wa taifa hilo kujadili kuhusu hali ya afya ya rais Biya, kukosoa utendakazi wake pamoja na maamuzi yanayofanywa na Ikulu ya rais.

Emmanuel amehudumu katika wadhfa wa mkuu wa majeshi mbali na kushikilia cheo kikuu katika wizara ya ulinzi nchini humo.

Rais Biya amekuwa mamlakani tangu 1982 na alishinda muhula wa nane kwenye uchaguzi mkuu mwaka uliopita.

Kuidhinishwa kwa mabadiliko haya ya kisheria nchini Cameroon kunatambulika kama tukio la kihistoria tangu mwaka 2008 ambapo taifa hilo lilishuhudia pingamizi za kisheria kutoka kwa wananchi baada ya bunge la kitaifa kuongeza hatamu ya uongozi wa rais na kusababisha maandamano makubwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending