Connect with us

News

Achani, Aagiza wizara 10 zilizogatuliwa kupeana kandarasi kwa Vijana

Published

on

Gavana wa kaunti ya Kwale Fatuma Achani ameagiza wizara 10 zilizogatuliwa katika serikali za kaunti kupeana kandarasi za kutekeleza miradi ya maendeleo kwa makundi ya akinamama na vijana katika kaunti hiyo ili kukabiliana na suala la ukosefu wa ajira na kupunguza viwango vya umaskini.

Kulingana na Gavana Achani, kufikia sasa jumla ya kampuni 300 za akina mama na vijana zimesajiliwa huku kampuni 105 zikipewa kandarasi za ujenzi wa zahanati, shule za Chekechea, upanuzi wa mabomba ya maji miongoni mwa kandarasi zengine.

Gavana Achani alisema hatua hiyo itasaidia wakaazi wa Kwale kujiajiri na kupunguza viwango vya umaskini.

“Nilisema akina mama na vijana waunde kampeni ili tuweze kujiajiri kwani hali ya uchumi kwa sasa hivi ni mbaya kwani saa hizi pale serikali ya kaunti imefikishwa haiwezi kuajiri na ni lazima tutafute njia mbadala za ni vipi watu watawezepata nafasi za ajira”, alisema Achani.

Gavana Achani awakabidhi vijana cheti cha usajili wa kampuni.

Kwa upande wake Katibu wa Wizara ya Huduma za Jamii na Ukuzaji Talanta katika serikali ya kaunti ya Kwale Riziki Mwasoza alisema kuwa wamekuwa wakiwapa mafunzo kina mama na vijana waliosajili kampuni na kuwajimiza kutumia kampuni hizo kusaka zabuni katika mashirika ya kibinafsi.

“Kama idara mwaka uliopita tuliwafanyia mafunzo akinamama na vijana ya siku tatu ili kujua jinsi ya kusimamia mapato yao”, alisema Mwasoza.

Nao wakaazi ambao wanamiliki kampuni na waliofaidika na kandarasi za serikali ya Kwale wakiongozwa na Mathew Kailu kutoka Shimbahills alieleza kwamba tangu wasajili kampuni hizo wamepata zabuni za hadi shilingi milioni 9 zinazowapa faida kubwa na kufanya miradi mbali mbali ya kuwajimu kimaisha.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending