Connect with us

News

Catherine Kenga ndiye spika mpya wa bunge kaunti ya Kilifi

Published

on

Catherine Kenga amechaguliwa kuwa spika wa bunge la kaunti ya Kilifi katika kikao maalum ambacho kiliandaliwa katika bunge hilo Jumatu Julai 21 2025.

Katika kikao hicho kilichoongozwa na naibu spika wa bunge hilo Naftal Kombo kwenye majengo ya bunge hilo mjini Malindi, Catherine Kenga alipata jumla ya kura 41, akifuatwa na wakili Faith Zawadi Kingi aliyepata kura 6 huku kura moja ikiharibika.

Wawakilishi wadi watatu walikosa kuhudhuria kikao hicho ingawa sababu za viongozi hao kukosa  kuhudhuria hazikuwekwa bayana.

Kenga anachukua hatamu ya kuliongoza bunge hilo kutoka kwa aliyekuwa spika Teddy Mwambire ambaye alitimuliwa  mapema mwezi uliopita Juni 30, 2025 kupitia kura ya maoni.

Mwambire alibanduliwa kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na ukiukaji wa katiba.

Catherine  ni miongoni mwa wagombeaji wanne waliotuma maombi ya kuwania wadhifa huo baada ya kujiuzulu kama waziri wa barabara katika serikali ya Kaunti ya Kilifi chini ya uongozi wa gavana Mung’aro.

Pichani:Kutoka kushoto,Karani wa bunge la kaunti ya Kilifi, Micheal Ngala, gavana Gedion Maitha Mung’aro na spika wa Sasa Catherine Kenga (Picha Kwa hisani

Catherine Kenga atakuwa spika wa tatu kulihudumia bunge hili, baada ya spika wa kwanza Jimmy Kahindi ambaye alihudumu kwa vipindi viwili chini ya uongozi wa gavana Amason Kingi ,ambaye sasa ni spika wa bunge la seneti.

Teddy Mwambire ndio alichukua wadhifa huo baada ya uchaguzi mkuu wa 2022, aliposhindwa na Kenneth Kazungu  Charo almaarufu ‘Tungule’ katika kinyang’anyiro  cha ubunge  wa  Ganze.

Catherine Kenga sasa anajukumu la kuleta mshikmano katika bunge hilo linalokabiliwa na mgawanyiko  kati ya wandani wa gavana Mung’aro kwa upande mmoja na wale ambao walimuunga mkono Teddy Mwambire wakati kura ya kutokuwa na imani naye ilipopigwa.

Kuwepo kwa maafisa wa ngazi za juu kutoka  serikali ya gavana Mungaro wakati wa kura hiyo ni ishara ya wazi kwamba spika wa sasa Catherine Kenga ana usuhuba na serikali ya sasa ya  gavana Mung’aro.

Hata hivyo, kura hiyo ilipigwa licha ya kuwepo kwa agizo la mahakama lililotolewa  wiki mbili zilizopita  kusitisha mipango ya kumtimua Teddy Mwambire hadi kesi iliyowasilishwa mahakamani kusikilizwa na kuamuliwa.

Miongoni mwa walioshiriki kura hiyo ni pamoja na Tendai Mtana Lewa, na Mazera Shadrack.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending