Connect with us

News

Chibule, ahimiza wakaazi kutoa damu kusaidia wagonjwa wa Selimundu

Published

on

Wizara ya afya kaunti ya Kilifi imefichua kwamba maradhi ya Selimundu ni miongoni mwa maradhi ambayo yanaathiri idadi kubwa zaidi ya wakaazi kaunti hiyo.

Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Afya kaunti hiyo Peter Mwarogo, mkurugenzi wa afya kaunti ya Kilifi Leli Hassan alisema kwamba kila siku zaidi ya watu kumi hupatikana wakiugua maradhi hayo kaunti ya Kilifi.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya maradhi hayo ya Selimundu katika uwanja wa Vipingo eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, wizara hiyo imesema kwamba asilimia sitini ya maradhi hayo yameathiri wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kusini.

Kauli hiyo iliungwa mkono na Naibu Gavana kaunti ya Kilifi Florah Mbetsa Chibule ambaye alisisitiza haja ya wakaazi kujitokeza na kutoa damu kwa hiari ili kuhakikisha wanasaidia waathiriwa wanaougua maradhi ya Selimundu.

Wananchi wakishiriki maandimisho ya siku ya Selimundu

Vile vila Chibule alisitiza haja ya wakaazi kujisahili kwenye mpango wa bima ya Kitaifa ya afya SHA ili kupata matibabu ya gharama ya chini wanapotaka dharura ya kiafya.

Naibu gavana huyo alisistiza jamii kaunti hiyo kuondoa unyanyapaa kwa waathiriwa wa maradhi hayo huku akishinikiza hamasa kwa jamii kuhusu kwa watu wanaoishi na maradhi hayo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ya jamii Bashir Isaak akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya nchini Aden Duale, alisema eneo la pwani na magharibi mwa nchi ndiyo yaliyosajili idadi kubwa ya wanaoishi na maradhi hayo.

Bashiri alipendekeza wahudumu wa afya nyanjani kupewa mafunzo maalumu ya kuhakikisha wanatambua sawa na kuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa waathiriwa wa maradhi hayo hasa maeneo ya mashinani.

Alisistiza haja ya waathiriwa wa maradhi hayo na umma kwa ujumla kujisajili kwenye mpango wa bima ya matibabu ya afya wa SHA ili kuwagharamia matibabu kwani baadhi ya wanaougia maradhi hayo hawana uwezo wa kimatibabu sawa na kununua dawa.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending