News
Chibule, ahimiza wakaazi kutoa damu kusaidia wagonjwa wa Selimundu
Wizara ya afya kaunti ya Kilifi imefichua kwamba maradhi ya Selimundu ni miongoni mwa maradhi ambayo yanaathiri idadi kubwa zaidi ya wakaazi kaunti hiyo.
Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Afya kaunti hiyo Peter Mwarogo, mkurugenzi wa afya kaunti ya Kilifi Leli Hassan alisema kwamba kila siku zaidi ya watu kumi hupatikana wakiugua maradhi hayo kaunti ya Kilifi.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya maradhi hayo ya Selimundu katika uwanja wa Vipingo eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, wizara hiyo imesema kwamba asilimia sitini ya maradhi hayo yameathiri wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kusini.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Naibu Gavana kaunti ya Kilifi Florah Mbetsa Chibule ambaye alisisitiza haja ya wakaazi kujitokeza na kutoa damu kwa hiari ili kuhakikisha wanasaidia waathiriwa wanaougua maradhi ya Selimundu.

Wananchi wakishiriki maandimisho ya siku ya Selimundu
Vile vila Chibule alisitiza haja ya wakaazi kujisahili kwenye mpango wa bima ya Kitaifa ya afya SHA ili kupata matibabu ya gharama ya chini wanapotaka dharura ya kiafya.
Naibu gavana huyo alisistiza jamii kaunti hiyo kuondoa unyanyapaa kwa waathiriwa wa maradhi hayo huku akishinikiza hamasa kwa jamii kuhusu kwa watu wanaoishi na maradhi hayo.
Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ya jamii Bashir Isaak akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya nchini Aden Duale, alisema eneo la pwani na magharibi mwa nchi ndiyo yaliyosajili idadi kubwa ya wanaoishi na maradhi hayo.
Bashiri alipendekeza wahudumu wa afya nyanjani kupewa mafunzo maalumu ya kuhakikisha wanatambua sawa na kuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa waathiriwa wa maradhi hayo hasa maeneo ya mashinani.
Alisistiza haja ya waathiriwa wa maradhi hayo na umma kwa ujumla kujisajili kwenye mpango wa bima ya matibabu ya afya wa SHA ili kuwagharamia matibabu kwani baadhi ya wanaougia maradhi hayo hawana uwezo wa kimatibabu sawa na kununua dawa.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali
Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.
Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.
Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.
Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.
Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.
Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.
Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa
Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.
Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.
Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.
“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

