Sports
Florian Wirtz Sasa Ni Mali Ya Liverpool
Ni Rasmi kwamba kilabu ya Liverpool imetangaza kupata sahihi ya kiungo wa taifa la Ujerumani na kilabu ya Bayern Leverkusen Florian Wirtz kwa dau la Euro milioni 150.
Mchezaji huyo anakua sajili wa pili kwa kocha Arne Slot na mchezaji ghali katika historia ya kilabu hiyo na miongoni mwa wachezaji 10 waliosajiliwa na donge nono zaidi barani ulaya nyuma ya Neymar na Mbappe ambao wote sajili zao zilikua za kihistoria.
Tineja huyo mwenye umri wa miaka 22 alishinda mataji matatu msimu wa mwaka 2023/24 chini ya kocha Xabi Alonso akifanikiwa kucheka na wavu mara 57 kutoka mechi 197 na kupiga pasi 65 kwa wenzake.
Wirtz anakua ndiye mchezaji ghali wa taifa la ujerumani na ligi ya Bundesliga akiwa pia ghali kusajiliwa ligi ya Epl.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

