Connect with us

News

Gachagua: Upinzani hauna nia ya kupindua serikali

Published

on

Aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua amekanusha madai kwamba mrengo wa upinzani unapanga kumuondoa rais William Samoei Ruto madarakani.

Katika taarifa yake ya siku ya Jumatano terehe 9 mwezi Julai, 2025 kwa vyombo vya habari, muda mfupi baada ya hotuba ya rais Ruto, Gachagua alisema vuguvugu la ONE TAM halina nia ya kuchukua mamlaka kwa njia ambayo sio halali.

Gachagua alimtaka rais Ruto kutekeleza majukumu yake ipasavyo na pia kudhibiti visa vya vya watu kutekwa nyara na kuuliwa katika mazingira tatanisha.

Gachagua pia alimkosoa rais Ruto akisema amekuwa akipuuza kilio cha wananchi hali ambayo inawafanya Wakenya wengi kuendelea kuhangaika.

‘’Bwana Ruto punguza hasira na kwa unyenyekevu mwingi nakushauri kwamba hasira sio suluhu maana haitakusaidia. Unapaswa kujua nini unapaswa kufanya maana haujakuwa ukiwasikiza Wakenya’’ alisema Gachagua.

Wakati huo huo, Gachagua ambaye pia ni Kinara wa chama cha DCP aliibua madai kwamba Rais Ruto amekuwa akiwatumia wahalifu kuharibu mali ya watu wakati maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z ambao wamekuwa wakiandamana nchini kuwasilisha matakwa yao kwa serikali.

‘’Siku ya Sabasaba wahalifu hao walipeleka maandamano maeneo mbalimbali nchini hasa eneo la Mlima Kenya na yale mengine ambayo yanakashifu uongozi wa serikali kuu’’ aliongeza Gachagua.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending