Connect with us

News

Kalonzo, Gachagua Wapinga Ujenzi wa Kinu cha Nuklia Kilifi

Published

on

Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, wamepaza sauti kupinga ujenzi wa kinu cha Nuklia katika eneo la Uyombo wadi ya Matsangoni Kaunti ya Kilifi.

Wakihutubu mjini Malindi Kaunti ya Kilifi viongozi hao akiwemo kinara wa DCP, aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua na mwenzake wa DAP, Eugene Wamalwa, waliongeza kwamba tayari wamewaagiza mawakili kuwasilisha kesi mahakamani kupinga mradi huo.

Waliyasema haya baada ya kuhudhuria misa ya Jumalipili katika katika Kanisa la JCC iliyoongozwa na Askofu Kakala mjini humo katika siku ya pili ya ziara yao ya ukanda wa Pwani.

Kalonzo alizidisha makombora yake Kwa serikali ya Rais William Ruto akiitaka iwajibikie maovu yake ya visa vya utekaji nyara na mauaji ya Vijana wa kizazi cha Gen-Z wakati wa Maandamano mwaka uliopita.

Kiongozi huyo alisema kwamba mnamo tarehe 25 mwezi huu wa Juni 2025, upinzani utawaongoza wakenya kuwakumbuka vijana waliouawa wakati wa Maandamano hayo ya Gen-Zs mwaka uliopita, kwa kuwasha mishumaa nje ya majengo ya bunge.

Kiongozi wa DCP, na aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua alisema serikali ya Kenya Kwanza, inaendelea kupora pesa za wafanyi kazi kutoka hazina ya malipoa ya Uzeeni NSSF, na kuzitumia Kwa miradi ya kibinafsi katika eneo la Bomas.

Picha kwa hisani

Kwa upande wake Kiongozi wa DAP, Eugene Wamalwa alisema kwamba serikali ya Rais Ruto sasa inatumia pesa za ushuru wa nyumba kujenga masoko katika Kaunti mbali mbali kama njia Moja wapo ya mbinu za kuwashawawishi viongozi hasa Magavana,kuunga mkono serikali ya KK, na kuongeza Kwamba ujenzi wa masoko ni jukumu la serikali za ugatuzi.

Viongozi hao waliwahutubia wananchi katika soko la Kwajiwa mjini Malindi, huku msafara huo ukisimama eneo la Matsangoni, Chuo kikuu Cha Pwani mjini Kilifi, na mji wa Mtwapa.

 

Taarifa ya Eric ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Baraza la Jamii ya Sekuye lalamikia uchimbaji wa madini kiholela

Published

on

By

Baraza la Wazee wa jamii ya Sekuye eneo la Moyale kaunti ya Marsabit limejitokeza na kulalamikia kuharibiwa kwa mazingira ya maeneo yao hasa katika kijiji cha Dabel kutokana na uchimbaji madini kiholela.

Wazee hao wamewalaumu viongozi wao ikiwemo serikali ya kaunti kwa kulinyamazia suala hilo huku wakaazi wakiendelea kunyanyaswa raslimali zao.

Baraza hilo, chini ya Katibu wake mkuu Haji Hassan Tepo, limedai kwamba uchimbaji huo wa madini kiholela, unyakuzi wa ardhi, unyanyasaji wa jamii umechangiwa na baadhi ya wawekezaji kutoka taifa Jirani la Somalia na Ethiopia ambao hawana vibali halali.

Hassan aliimtaka serikali kupitia Waziri wa madini nchini Hassan Ali Joho kuingilia kati suala hilo na kuhakikisha uchumbaji wa madini katika kijiji cha Dabel unasitishwa kwani wawekezaji zaidi ya 20 wamebuni makundi na kuendelea kuwanyanyasa wenyeji.

Hassan aliweka wazi kwamba baraza hilo pamoja na jamii ya Sekuye linapinga mpango huo na kusisitisha kwamba hawatakubali ardhi yao wanayoitegemea kwa shughuli mbalimbali kutumika vibaya.

Naibu Mwenyekiti wa baraza hilo Abdukadir Dilo alisema hali hiyo imewasabibishia hasara kwani mifugo imeangamia, uchumi wa kijiji hicho ukididimia zaidi na akamtaka rais Ruto kuingilia kati kwani licha ya Waziri Murkomen kufunga uchumbaji kufuatia utovu wa usalama bado wawekezaji kutoka Ethiopia na Somali wamekuwa wakiendeleza mpango huo.

Wazee hao hata hivyo walisisitiza kwamba hawatakubali kuachilia ardhi yao kunyakuliwa na watu wanaodai kuwa wawekezaji ilhali vijana wa eneo hilo hawana kazi, huku wanafunzi wakiacha shule na zaidi ya akina mama 22 wakiachwa na wanaume zao kufuatia suala hilo katika kijiji cha Dabel.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Murkomen ahimiza ushirikiano wa pamoja na wadau wa masuala ya ubaharia

Published

on

By

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen, ametoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya washirika na wadau ili kuimarisha usalama wa baharini na maziwa makuu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano la kamati ya uongozi wa Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS) lililofanyika mjini Mombasa, Waziri huyo alisisitiza kuwa ushirikiano wa mapema ni muhimu katika kukabiliana na vitisho vinavyoibuka vya usalama wa baharini.

“Ushirikiano wa mapema na muhimu katika kulinda usalama wetu wa baharini,” alisema Murkomen.

Kongamano hilo la siku tatu linaandaliwa kwa pamoja na huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya (KCGS) pamoja na mradi wa njia muhimu za baharini wa Indo-Pasifiki unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU-CRIMARIO), ukiwaleta pamoja wadau wa usalama wa baharini..

Mradi wa EU-CRIMARIO umeundwa kuimarisha usalama na ulinzi wa baharini kupitia kuboreshwa kwa ushirikiano wa taarifa na uratibu wa operesheni.

Kongamano la siku tatu la kamati ya uongozi la Jukwaa la ushirikiano wa taarifa ya kanda ya Indo-Pasifiki (IORIS), Mombasa

Mpango wake mkuu, IORIS, ni jukwaa salama na lisiloegemea upande wowote linalotumia mtandao, unaounganisha zaidi ya mashirika 150 kutoka nchi 70, na kuwezesha uratibu wa operesheni za baharini kwa wakati halisi.

Kauli za Murkomen ilijiri kufuatia tangazo la Rais William Ruto kwamba kampuni ya usafiri wa baharini ya Norway, Wilhelmsen, itaajiri mabaharia 1,000 kutoka Kenya, baada ya mazungumzo na kampuni hiyo.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mkurugenzi wa EU-CRIMARIO Martin Cauchi Inglott, Mkurugenzi mkuu wa huduma ya walinzi wa Pwani ya Kenya Bruno Shioso, Naibu mkuu wa ujumbe wa umoja wa Ulaya nchini Kenya Ondrej Simek, pamoja na washkadau wengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending