News
Kenya Police Bullets Mabingwa KWPL
Kilabu ya akina dada Kenya Police Bullets ndiyo mabingwa wa ligi ya taifa akina dada kwpl baada ya kuwanyuka Trinity starlets magoli 4-0 mechi ya mwisho hapo jana ugani afraha stadium Nakuru
Winga matata Emily Kemunto moranga alifungua ukurasa wa magoli dkaika 40,kisha Mshambulizi matata Rebecca Becky Okwaro akifunga magoli matatu dakika ya 55 ,dakika ya 79 na dakika 89 na kuchukua kiatu cha dhahabu kwa kufunga magoli 16 msimu huu
Kocha wa Bullets Beldine Odemba hakuficha furaha yake baada ya kushinda kombe hilo kwa mwaka wa pili mfululizo akitaja kwamba upinzani ulikua mkali ila wasichana wake wamepigana mpaka siku ya mwisho kubeba taji hilo.
Katika matokeo mengine
Kisped Queens 2-1 Vihiga Queens
Bunyore Starltes 0-3 Bungoma Queens
Kibera soccer Women 7-0 Mombasa olympic
Ulinzi Starlets 4-0 Kisumu All Starlets
JEDWALI
Bullets alama 46
Ulinzi starlets 45
Kibera soccer alama 42
Kayole starlets ni mabingwa wa KWNSL Baada ya kunyuka kayolets 3-0 madira soccer assasin
Iron ladies 3-0 Diani Quens na kushinda taji la fkf divisheni ya kwanza.
News
NCTC yaanzisha hamasa mashinani kudhibiti ugaidi
Kituo cha kitaifa cha kukabiliana na ugaidi yaani National Counter Terrorism Centre (NCTC) kimeanzisha mpango wa kutoa hamasa za kuwaepusha wananchi na masuala ya ugaidi hasa maeneo ya Shakahola katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Akizungumza katika eneo hilo, Afisa mkuu wa kituo hicho Grace Kaparo aliwataka wazazi kufuatilia kwa ukaribu mienendo ya watoto wao kama njia mojawapo ya kuzuia michipuko ya makundi ya ugaidi.
Kaparo alidokeza kwamba mpango huo unalenga kupunguza visa vya uhalifu miongoni mwa vijana sambamba na kuwajengea mustakabali bora wa maisha yao.
Hamasa hiyo inajiri baada ya kushughudiwa maafa ya watu zaidi ya 400 katika msitu wa Shakahola kutokana na mafunzo ya itikadi kali huku mshukiwa mkuu wa mauaji hayo akiwa katika mikono ya maafisa wa polisi.
“Tumekuja Shakahola kuelimisha jamii kuepusha makundi ya kigaidi na jinsi ya kutambua watu walio na itikadi kali ili kuepusha watu kuangamia kama hapa Shakahola watu wangekuwa na ufahamu wangeepuka maafa”, alisema Grace.
Kwa upande wake Naibu Kamishna eneo Malindi kaunti ya Kilifi Harrison Matevwa aliwataka maafisa wa utawala eneo hilo kuendeleza hamasa za mara kwa mara kwa wakaazi wa maeneo yao ili kutathmini changamoto zinazowakumba na kuzitatua mara moja.
“Naiambia kamati ya usalama eneo hili kutembea na kufanya baraza za usalama kuweza kuskia ile wananchi wanapitia kwa sababu wengi wanakosa usaidizi ndio watu wahalifu wakija wanaweza kuwapotosha”alisema Harrison.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wakurugenzi wa Kampuni ya Bima ya Direct Line waagizwa kufika Mahakamani
Mahakama ya Malindi imewaamuru wakurugenzi wa Kampuni ya Bima ya Direct Line kufika Mahakamani binafsi kwa ajili ya kuhojiwa.
Hii ni baada ya kampuni hiyo kushindwa kutekeleza amri ya Mahakama ya kulipa fidia ya shilingi milioni 2.26 kwa mwanamke aliyejeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani iliyokea Oktoba 6, mwaka 2016.
Kampuni hiyo, inayohusishwa na familia ya mfanyabiashara mashuhuri nchini ilishindwa kumlipa Hellen Waiyaki kiasi cha shilingi 2,259,825 kama ilivyoamriwa na Mahakama.
Waiyaki aliwasilisha kesi Mahakamani baada ya kampuni hiyo kukosa kutekeleza wajibu wake wa kulipa kiwango hicho cha pesa licha ya kuagizwa na Mahakama kufuatia ajali hiyo iliyohusisha basi la Tahir Sheikh Said Transporters Limited, maarufu kama TSS Bus Company, yenye nambari ya usajili KBZ 475S.
Akitoa uamuzi huo, Hakimu Mwandamizi wa Mahakama ya Malindi, Joy Wesonga, alisema ni lazima wakurugenzi hao wafike Mahakamani binafsi na kujieleza, akisema kampuni hiyo imekuwa ikiwazuia wananchi kufikia ofisi zao.
“Wakurugenzi hao watahitajika kufika mahakamani wakiwa na kuwasilisha vitabu vya hesabu vilivyokaguliwa vya kampuni, taarifa za benki pamoja na sajili ya mali za kampuni kwa kipindi cha miaka miwili ya mwisho ya kifedha ili Mahakama iweze kubaini uwezo wa kifedha wa kampuni hiyo na hali ya shughuli zake za kibiashara nchini Kenya.” alisema Hakimu Wesonga.
Katika hati kiapo kilichowasilishwa mahakamani kupitia wakili wake George Wakahiu, Hellen Waiyaki alisema alikuwa abiria ndani ya gari hilo ambalo lilikuwa likiendeshwa kwa uzembe kabla ya kupinduka na kusababisha ajali iliyomwacha na majeraha mabaya mwilini.
Kesi hiyo itaendeleza mnamo Julia 31 mwaka huu
Taarifa ya Mwanahabari wetu

