Business
KPA inamatumaini bandari ya Mombasa kuimarika zaidi
Mkurugenzi mkuu wa halmashauri ya bandari nchini, nahodha William Ruto, ameibua matumaini mapya kuhusu uboreshaji wa Bandari ya Mombasa baada ya kutangaza hatua mbalimbali za kisasa zinazolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za bandari.
Akizungumza kwenye kikao na viongozi wa chama cha mawakala wa forodha nchini (KIFWA), nahodha Ruto alisema KPA imeanza kutekeleza miradi muhimu kama kudhibiti kina cha bahari kwa ajili ya kupokea meli kubwa, ujenzi wa Gati ya kwanza katika eneo la Dongo Kundu, pamoja na uendelezaji wa Gati 19B ili kupanua uwezo wa bandari ya Mombasa kushughulikia mizigo zaidi.
Alieleza kuwa KPA pia imewekeza kwenye mitambo ya kisasa yenye ufanisi wa nishati, ikiwemo kreni za ‘rubber-tyred gantry’, hatua ambayo itapunguza muda wa meli kukaa bandarini na kuongeza kasi ya kazi.
Katika hatua nyingine, Ruto alisema utekelezaji wa mifumo ya kiotomatiki utaongeza kasi ya huduma hususan kwenye lango la bandari, akibainisha kuwa mageuzi ya kidijitali ndiyo dira ya kufanikisha shughuli za bandari kwa viwango vya kimataifa.
Pia alisisitiza umuhimu wa bandari ya Lamu, akisema kituo hicho kinazidi kuimarika kama nguzo muhimu ya mradi wa LAPSSET, huku akialika viongozi wa KIFWA kufanya ziara ya kujifunza kwenye bandari hiyo.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa KIFWA kanda ya Pwani, Rajab Hamisi, aliwapongeza wanachama kwa kazi yao thabiti, na kuishukuru KPA kwa kuendeleza ushirikiano unaolenga kuongeza ushindani na ufanisi katika sekta ya usafirishaji.
Taarifa Mwanahabari wetu.
Business
Wafanyibiashara wa mitumba eneo la Diani wafunga biashara zao
Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Diani, kaunti ya Kwale, wamelazimika kufunga biashara zao kutokana na kudorora kwa shughuli za kibiashara katika kipindi hiki cha msimu wa watalii wachache na mvua zinazoendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
Wafanyabiashara hao wanasema idadi ya wanunuzi imepungua kwa kiasi kikubwa, hali iliyosababisha nguo nyingi kukosa soko.
Kulingana na wafanyibiashara hao wanategemea zaidi watalii wa ndani na nje na kutokana na msimu huu kuwa uko uko chini wateja wamepungua hali inayofanya maisha kuwa mgumu.
Wanasema wamelazimika kutupa baadhi ya nguo kwani zimesalia sokoni kwa muda mrefu hadi zingingine kuharibika, jambo ambalo limepelekea kupata hasara kubwa.
Aidha, wameongeza kuwa bei ya nguo za mitumba imeendelea kupanda ambapo wananunua ngunia moja kwa shilingi elfu 40 huku mauzo yakizidi kushuka.
“ Biashara imedorora sai kwani hakuna wateja ikizingatiwa kuwa tunategemea sana watalii na sasa hakuna wageni hata imetulazimu kutupa nguo kwani ngigi zimeharibika baada ya kukaa kwa mda mrefu bila kununuliwa”.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mamlaka ya AFA yahimiza upanzi wa mkorosho
Mamlaka ya Kilimo na Chakula nchini AFA, imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha taifa linaboresha mazao yake na kuchangia uzalishaji wa chakula nchini.
Hatua hii imechangia zaidi na mikakati endelevu ya kuwawezesha wakulima kufahamu mipango endelevu ya uimarishaji wa Kilimo cha sasa na kwa kuzingatia utumiaji wa mifumo bora ya kilimo.
Mamlaka hiyo ambapo inaendeleza kampeni ya kuhamisha wakulima kuhusu umuhimu wa kilimo cha Korosho imesisitiza haja ya ujumuishaji wa wakulima, wawekezaji na wadau mbalimbali ili kupiga jeki sekta ya Kilimo huku ikiahidi kuendeleza hamasa kwa jamii za kaunti za Pwani kuhusu kilimo cha korosho na utafutaji wa soko huru.
Katika Kongamano la kitaifa lililoandaliwa katika kaunti ya Kwale, Mamlaka hiyo iliwapa wakulima kutoka kaunti sita za Pwani miche ya mikorosho elfu mia moja katika juhudi za kukuza kilimo cha zao hilo nchini.
Katibu katika Idara ya Kilimo nchini Paul Kiprono, alisema mpango huo unalenga kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji wa korosho na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, Kiprono alitoa wito kwa serikali za kaunti pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kushirikiana kwa karibu ili kuboresha kilimo cha korosho.
“Kenya ilikuwa ikiongoza katika zao la mkorosho katika miaka ya 1990 lakini kutokana na changamoto za kibiashara zao hilo lilishuka katika masoko ya kimataifa kutokana na ukosefu wa kuwekezaji kwa wakulima lakini sasa tumeanza kupiga hatua kwani tunazalisha zaidi ya tan elfu 9 za korosho”, alisema Rono.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa AFA, Cornelly Serem, alisema mamlaka hiyo imejizatiti kuboresha kilimo cha korosho kupitia utoaji wa miche bora na mafunzo kwa wakulima ili kuongeza tija.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

